Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu Akutana na kuzungumza viongozi wa dini ya kiislam katika ukumbi wa Bwalo la maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es salaam.

 

 Mkuu wa Jeshi la Polisi  nchini IGP Ernest Mangu  akisalimiana na masheikh wa mikoa na maimamu wa misikiti katika ukumbi wa bwalo la maafisa wa Polisi wakati wa   kikao cha muendelezo wa  kampeni ya familia yetu haina mhalifu kilichoratibiwa na taasisi ya kiislamu ya Mwinyi  Baraka. Picha na Hassan Mdeme- wa Jeshi la Polisi
Mkuu wa Jeshi la Polisi  nchini IGP Ernest Mangu  akiwa na  Mufti na Sheikh mkuu wa Tanzania Shabani Simba na viongozi wengine wa dini ya kiislamu wakati wakiingia katika ukumbi wa bwalo la maafisa wa Polisi kuhudhuria   kikao cha muendelezo wa  kampeni ya familia yetu haina mhalifu kilichoratibiwa na taasisi ya kiislamu ya Mwinyi  Baraka.
--
Na Tamimu Adam – Jeshi la Polisi
Viongozi  wa dini wametakiwa kuendelea  kufanya  doria za kimwili na kiroho  katika kuimarisha ulinzi na usalama ndani ya jamii ikiwa ni pamoja na  kuwajenga vijana  katika maadili mema na kuacha kutenda dhambi  ya kujihusisha na vitendo vya uhalifu.
Rai hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu alipokutana na viongozi wa dini ya kiislam katika ukumbi wa Bwalo la maafisa wa Polisi Oysterbay, jijini Dar es salaam. Kikao hicho kiliratibiwa na taasisi ya kiislamu ya Mwinyi Baraka inayoongozwa na Sheikh Issa othuman.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top