Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TUNDA MAN na NYOTA NDOGO sasa ni kupika na kupakuwa: picha za kimahaba za zanaswa wakiwa katika mapozi ya kimahaba ! yadaiwa kila akienda kenya huwa analala nyumbani kwa nyota ndogo!!


 Memba wa Kundi la Tip Top Connection , Khalid Ramadhan ‘Tunda Man’ akipozi kimahaba na mwanamuziki Mwanaisha Abdallah ‘Nyota Ndogo’.


Memba wa Kundi la Tip Top Connection lenye maskani yake Manzese jijini Dar, Khalid Ramadhan ‘Tunda Man’ na mwanamuziki wa nchini Kenya, Mwanaisha Abdallah ‘Nyota Ndogo’ wamenaswa laivu wakiwa kwenye pozi la mahaba niue.




Kwa mujibu wa chanzo chetu makini kutoka nchini humo, wawili hao walikuwa wakijiachia nyumbani kwa Nyota Ndogo huku kukiwa na madai mazito kuwa eti wanapika na kupakuwa. 
‘Tunda Man’ na ‘Nyota Ndogo’ wakila ujana.
Ilidaiwa kwamba Tunda Man anapokwenda Kenya huwa anafikia nyumbani kwa Nyota Ndogo. “Wasanii wengi wanakuja Kenya wanajifanya kuja kufanya shoo kumbe wanawafuata wanawake zao ila mimi namsihi Tunda Man ajiangalie, yasije yakamkuta kama ya wasanii wengine walivyopewa masaa ishirini na nne wasikanyage Kenya tena,” kilisema chanzo hicho.
Baada ya kupata maelezo hayo, paparazi alimvutia waya Tunda Man na kumpa hongera ya kummiliki Nyota Ndogo ambapo alikuja juu na kudai kuwa anahisi anataka kuchafuliwa.
“Kaka nadhani unajua kuwa nina mke na sijawahi kupata skendo kubwa kama hiyo, Nyota Ndogo namheshimu kama dada yangu na sijawahi hata kufikiria kumtongoza please achana na hiyo habari,” alijitetea Tunda Man bila kujua tuna picha zao za mahaba.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top