Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wanafunzi 9946 hawajapatiwa fedha ya mafunzo kwa vitendo

               



Serikali imesema ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya fedha za malipo ya mafunzo kwa vitendo kwa mwaka wa masomo 2013 2014.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi Habari, Elimu na Mawasiliano Cosmas Mwaisobwa wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.(Martha Magessa)

Mwaisobwa alisema kuwa jumla ya wanafunzi 9946 kutoka vyuo vikuu vitano hawajapatiwa fedha kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo ambao wengi wao tayari wako katika maeneo waliyopangiwa.
"Bodi tayari imeandaa malipo yao na yanatarajiwa kutumwa mwishoni mwa juma hili, ambapo vyuo vikuu vitano ikiwemo Tumaini Makumira (TUMA) wanafunzi 1 715, Stefano Moshi (SMMUCO) wanafunzi 1 191, Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM)wanafunzi 2 578, Mt. Augustino (SAUT) wanafunzi 2639 na Teofilo Kisanji (TEKU) wanafunzi 1823.
Akijibu swali la waandishi wa Habari Mwaisobwa alisema kuwa sababu zilizopelekea kuchelewa kwa fedha hizo ni mchakato wa upatikanaji wa fedha zilitarajiwa kupatikana mapema zaidi.
Aidha, Mwaisobwa alitoa rai kwa wazazi na walezi wenye uwezo wa kuwalipia watoto wao wafanye hivyo ili kuwapa nafasi wale wasio na uwezo wa kunufaika na mkopo mkopo wa Bodi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top