Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ALIYEMUAA AFISA USALAMA WA TAIFA NAYE AUAWA NA POLISI JIJINI DAR

 

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgUk47sG0z6GjXhudvAgdiLNlK_QiLX_HJ6zVKqs054lL62j-39Cqz4drpKxSqIlvO5-rZJQmO8fabsEqw0yD0IeXMdi819n-tzGIYbnv7z6x-J_EDT6k6QudI2enuEIL9DpsRCWjto4PBo/s1600/001.JPG
Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, amethibitisha kuwa Jeshi lake limefanikiwa kumkamata jambazi sugu aitwaye Paulo Thamas Milanzi maarufu Chinga (35), Mmakonde mkazi wa Chanika.

Amesema baada ya majibizano ya risasi jambazi hilo lilijeruhiwa na kufikishwa hospitali ya Muhimbili kwa matibabu lakini baadaye alifariki dunia.

Alisema jambazi huyo lilikuwa akitafutwa na polisi kutokana kuhusika kwenye matukio ya mauaji na wizi ikiwemo tukio la kuuawa kwa Afisa Mwandamizi wa Usalama wa Taifa, Sylivabus Adrian Mzeru Aprili 29, 2014 liliotokea Uwanja wa Ndege.

Aliongeza kuwa Chinga alikamatwa na bastola aina ya Star.'

Majambazi wenzake walikamatwa na kwa sasa wako gerezani wakisubiri taratibu za kisheria kuchukua mkondo wake.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana
Back To Top