Rais Blaise Compaore aliyejiuzulu.
RAIS wa Burkina Faso, Blaise Compaore ametangaza kujiuzulu kufuatia vurugu za kisiasa zinazoendelea nchini humo.
Jenerali Honore Traore.
Katika
vurugu hizo, jana waandamanji walilichoma bunge la nchi hiyo wakipinga
Rais Blaise Compaore, aliyeiongoza nchi hiyo kwa miaka 27, kutaka katiba
ifanyiwe mabadiliko ili aweze kugombea tena nafasi hiyo mwaka kesho.
Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo, Jenerali Honore Traore ndiye amechukua nafasi hiyo kwa muda.
Post a Comment