Swaumu
Sadick akiwa hospitali baada ya kujifungua mtoto huyo. Kwa mujibu wa
shuhuda wetu, tukio hilo ambalo kwa sasa ni gumzo, lilijiri hivi
karibuni mishale ya saa 8:00 usiku kwenye Kituo cha Afya Cha Kijiji cha
Mlali kilichopo wilayani Mvomero mkoani hapa.
Katika tukio hilo, ilielezwa kwamba Swaumu alijifungua kiumbe huyo wa
ajabu anayedaiwa kuwa na mkia mrefu huku akiwa hana miguu.
Ilidaiwa kwamba baada ya kutokea kwa tukio hilo, baadhi ya ndugu
walishikwa na taharuki kubwa huku wengine wakitoa taarifa kwa
mwanahabari wetu ambaye alifunga safari kutoka mjini Morogoro na
kuwasili kwenye kituo hicho cha afya majira ya saa 12:00 asubuhi.
Post a Comment