Jeshi la polisi mkoani rukwa linawashikilia watu saba
hadi sasa, kwa tuhuma za kuhusika na kitendo cha kikatili cha kukata kiganja cha
mkono wa kulia, cha mtoto mwenye ulemavu wa ngozi Baraka Cosmas Lusambo mwenye
umri wa miaka sita, katika kitongoji cha kikonde kata ya kipeta wilaya ya
sumbawanga vijijini, ambapo pia katika tukio hilo wamemjeruhi mtoto huyo mkono
wa kushoto.
Kaimu
kamanda wa polisi wa mkoa wa rukwa kamishna msaidizi wa polisi Leons Rwegasira,
amesema
wamefanikiwa kuwakamata watu hao kufuatia msako mkali, mara tu baada ya kutokea
tukio hilo kwenye kitongoji hicho cha kikonde, ambacho kinakuwa na wakazi wakati
wa msimu wa kilimo na kiangazi watu wanahama tena, katika familia yenye watoto
wengine watatu wenye ulemavu wa ngozi.
ACP.Rwegasira pia amesema
kwenye msako huo mkali, wamefanikiwa kuwakamata watu wanane wanaojihusisha na
uganga wa jadi na upigaji wa ramli chonganishi, ambacho ni chanzo kikubwa cha
kusababisha vifo na kujeruhiwa watu wenye ulemavu wa ngozi kwa imani za
kishirikina.
Mtoto baraka na mama yake
mzazi wamelazwa kwene hospitali ya rufaa ya jijini mbeya, wakitibiwa majeraha
waliyoyapata wakati wa purukushani za kumshambuliwa mtoto huyo.
Post a Comment