Aliyekuwa mfanyakazi wa Clouds Media, Cynthia Maximillan, amejikuta akitiwa mbaroni kwa madai ya kutapeli mamilioni ya shilingi ya wafanyakazi wenzake na marafiki aliosoma nao.
Inadaiwa kuwa mrembo huyo alitiwa rumande kituo cha polisi Oysterbay,
baada ya kuwakusanya marafiki zake na kuwapa mchongo kuwa, kuna viwanja
vinapatikana huko Bagamoyo kwa shilingi mil 1.5 kupitia Chama cha
Mazingira Fukayosi.
Inasemekana kuwa baada ya kupewa fedha hizo mrembo huyo alianza
kuwaletea habari ambazo walikuwa hawazielewi na ndipo wakachukua uamuzi
wa kumshtaki kwa utapeli wake.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Clouds, Ruge Mutahaba, amedai kuwa
anaomba umma ujue kuwa mrembo huyo sio mfanyakazi tena wa kampuni hiyo
kwani aliachishwa kazi na yeye pia ni mhanga wa utapeli huo.



Post a Comment