Akiwa mjini Geneva, Rais Kikwete ameongoza vikao vya Jopo la Kimataifa Linalopendekeza Jinsi Dunia inavyoweza kukabiliana na majanga yajayo ya magonjwa ya milipuko ambalo kazi yake imeungwa mkono na nchi 21 ambazo zilichangia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola.
Miongoni
mwa mikutano ambayo Rais Kikwete ameiongoza katika Makao ya Umoja wa
Mataifa (UN) mjini Geneva ni pamoja na yeye na wanajopo wenzake kutoa
maelezo kuhusu maendeleo ya kazi yao kwa nchi ambazo zilichangia
mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola katika nchi za Guinea, Liberia na
Sierra Leone.
Nchi
hizo ambazo zimeunga mkono kazi ya Jopo hili katika mkutano huo ni
Venezuela, Umoja wa Ulaya (EU), Uholanzi, Finland, Shirikisho la Russia
(Russian Federation), Norway, China, Ubelgiji, India, Ujerumani,
Marekani, Uswisi, Canada, Brazil, Denmark, Uingereza, Israel, Benki ya
Maendeleo ya Afrika (AfDB), Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Dunia (WB),
Jamhuri ya Korea na Japan.



Post a Comment