Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Anthony Mavunde achukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Dodoma jijini.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Dodoma,Antony Mavunde akionesha fomu alizochukua za kugombea Ubunge katika jimbo hilo nje ya ofisi za Halmashauri ya Dodoma. 
 Mgombea wa nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Dodoma Mjini,Antony Mavunde akipungia mamia ya mashabiki wakati akielekea katika ofisi za Mkurugenzi wa Halmashauri ya Dodoma kwekuchukua fomu.
 Mavunde akifurahia jambo na Wafuasi wake.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Dodoma Mjini kupitia chama cha Mapinduzi,Antony Mavunde akikabidhiwa fomu na Afisa Uchaguzi wa Jimbo la Dodoma Elizabeth Gumbo jana Mjini Dodoma.
 
MGOMBEA wa nafasi ya ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)Anthony Mavunde amechukua fomu na kuahidi kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha analinda haki za wakazi wa mji wa Dodoma katika masuala ya ardhi.
 
Akizungumza na wanachi mara baada ya kuchukua fomu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) Mavunde amesema akipata nafasi ya kuwa mbunge kupitia nafasi hiyo atakuwa mjumbe wa bodi ya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu(CDA)hivyo atahakikisha mamlaka hiyo inaboresha maisha ya watu na sio kuyadidimiza.

Aidha ameahidi kuimarisha sekta ya michezo ambayo imepewa kisogo katika Mkoa wa Dodoma.Michezo hiyo ni Pamoja na Mpira wa pete,Kikapu,Mpira wa mikono na Riadha.,Mavunde alisema kama akipewa ridhaa ya kuwa Mbunge wa Dodoma basi suala la michezo kwake litakuwa ni la lazima na inapiga hatua.

"Mimi ni muumini wa michezo hivyo tofauti na soka nitatoa nafasi pia kwa michezo mingine ambayo imekuwa ikiipa sifa mkoa wa Dodoma ili vijana waweze kujikwamua na kuondokana na tatizo la ajira, "alisema

Alisema akipata nafasi ya kuwa Mbunge wa Dodoma basi cha kwanza atakachofanya ni kukutana na viongozi wote wa vyama vya michezo mkoani hapa ili kuweka kalenda za kisasa ambazo zitaendeleza michezo.

Mavunde alisema lengo lake lingine ni kuanzisha academic ya michezo ambayo itakuwa ikiwaandaa vijana jinsi ya kuwa wachezaji wa kulipwa katika miaka ya baadae pamoja na kuwatafutia soko la kwenda kuonyesha vipaji vyao nje ya Tanzania.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top