Katibu 
Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (kulia) akibadilishana 
hati ya makubaliano na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Egon 
Kochanke (kushoto) katika hafla ya utiaji saini wa mikataba 2 ya sekta 
za maji, afya na maliasili leo alhamisi (Agosti 13, 2015) Jijini Dar Es 
Salaam.
Katibu 
Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (wa kwanza kulia) akisaini
 hati ya makubaliano katika hafla ya utiaji saini wa mikataba 2 ya sekta
 za maji, afya na maliasili leo alhamisi (Agosti 13, 2015) Jijini Dar Es
 Salaam. Wa pili kulia ni Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Egon
 Kochanke.
Katibu 
Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile akiongea na baadhi ya 
viongozi wa Wizara hiyo, ujumbe wa ulioandamana na Balozi wa Ujerumani 
pamoja na waandishi wa habari mara baada ya utiaji saini wa mikataba 2 
ya sekta za maji, afya na maliasili leo alhamisi (Agosti 13, 2015) 
Jijini Dar Es Salaam.(VICTOR)
Balozi wa
 Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Egon Kochanke akiongea na baadhi ya 
viongozi wa Wizara ya Fedha, wajumbe kutoka Ujerumani pamoja na 
waandishi wa habari mara baada ya utiaji saini wa mikataba 2 ya sekta za
 maji, afya na maliasili leo alhamisi (Agosti 13, 2015) Jijini Dar Es 
Salaam.
Katibu 
Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (kulia) akiteta jambo na 
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. Egon Kochanke leo alhamisi 
(Agosti 13, 2015) Jijini Dar Es Salaam wakati wa hafla ya utiaji saini 
wa mikataba 2 ya sekta za maji, afya na maliasili.
Baadhi ya
 wajumbe wa ulioandamana na Balozi wa Ujerumani wakimsikiliza Katibu 
Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile (hayupo pichani) alipokuwa
 anaongea wakati wa hafla ya utiaji saini wa mikataba 2 ya sekta za 
maji, afya na maliasili leo alhamisi (Agosti 13, 2015) Jijini Dar Es 
Salaam.
Baadhi ya
 viongozi kutoka Wizara ya Fedha, wajumbe kutoka Ujerumani pamoja na 
waandishi wa habari waliohudhuria hafla ya utiaji saini wa mikataba 2 ya
 sekta za maji, afya na maliasili leo alhamisi (Agosti 13, 2015) Jijini 
Dar Es Salaam.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
Serikali 
ya Tanzania na Ujerumani zimetiliana saini mikataba miwili ya misaada 
yenye thamani ya jumla ya Sh. Bilioni 39. 1 ambazo ni sawa na Euro 
milioni 17 kusaidia sekta mbalimbali nchini.
Makubaliano
 hayo yamesainiwa leo jijini Dar es salaam kati ya Katibu Mkuu Wizara ya
 Fedha Dkt. Servacius Likwelile kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na 
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Egon Kochanke ili kuleta mafanikio 
na maendeleo katika.
Sekta zitakazonufaika na msaada huo uliotolewa na Serikali ya Ujerumani ni pamoja na sekta ya afya, maji na maliasili.
Aidha, 
Dkt. Likwelile amemhakikishia Balozi Kochanke na ujumbe wake kuwa msaada
 walioipa Serikali utatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuleta 
ufanisi na kuongeza nafasi za ajira na hatimaye kuchangia katika 
kuboresha uchumi nchini.
Kwa 
upande wake Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Egon Kochanke amesema 
kuwa serikali ya Ujerumani itaendelea kushirikiana na Tanzania kwa 
kuzingatia uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi hizo mbili.
Zaidi ya 
hayo, serikali hizo mbili zimesaini mkataba wenye thamani ya Euro 
milioni 10 ambazo ni sawa na bilioni 23 za kitanzania kuisaidia 
usimamizi wa hifadhi ya taifa ya Selous.

 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment