Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MBOWE: Ulofa na Upumbavu Wetu ni kwa sababu ya CCM


Mgombea wa Ukawa alieteuliwa kuwania Ubunge wa Jimbo la Nzega Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Charles Mabula (kulia) akipeana mkono na aliekuwa Mgombea wa nafasi hiyo kwa Jimbo la Nzega mjini, Mezza Leonard (kati) akiekubali kushindwa baada ya kupigwa kura ya wazi na wananchi wa Nzega Mjini, jana Septemba 6, 2015.Kushoto ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Mh. Freeman Mbowe.
 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, amesema ili umasikini unaowakabili Watanzania uweze kuondoka lazima washirikiane kuiondoa madarakani CCM.

Amesema ulofa na upumbavu wanaodaiwa kuwa nao Watanzania umesababishwa na Serikali ya CCM kwa kuwa haiwajali Watanzania.

Mbowe  alitoa kauli  hiyo jana alipohutubia mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Laini Polisi mjini Nzega, Mkoa wa Tabora  ambapo  pia alilazimika kuwapigisha kura za mikono wananchi wa Nzega waliohudhuria mkutano huo ili kutatua mvutano wa wagombea wa ubunge katika Jimbo la Nzega Mjini lililokuwa na wagombea wawili wa Ukawa.

Wakati wa kura hizo, mgombea wa Chadema, Charles Mabura, aliibuka mshindi dhidi ya mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Meza John.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top