Mwenegoha ameiambia FikraPevu kuwa amechukua hatua hiyo ili iwe funzo kwa waganga na wauguzi wengine wanaofanya manyanyaso ya kupokea rushwa na kunyanyapaa wagonjwa hospitalini hapo.
Mkuu huyo amesema alipofika hospitalini hapo saa kumi na mbili asubuhi alimkuta mganga huyo akiwa amelala ndipo akampigia simu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dkt. Maja Susuma, aliyefika na kumpatia matibabu mtoto huyo.
Vyanzo vyetu vya habari ndani ya hospitali hiyo vinaeleza kuwa Mkuu huyo wa wilaya amechukua hatua hizo baada ya kupigiwa simu na wazazi wa mtoto aliyefikishwa hospitalini hapo saa kumi za usiku ili kupatiwa matibabu lakini mganga wa zamu alikataa kumtibu.
Sababu zinazotajwa kuwa ndizo zilizosababisha mganga huyo kutomtibu mgonjwa huyo ni madai aliyoyatoa kuwa Mganga ambaye angeingia zamu asubuhi ndiye ambaye angepaswa kumhudumia mtoto huyo.
Chanzo chetu cha habari kimedokeza kuwa, mhudumu huyo wa afya anatuhumiwa kwamba alikuwa amekwenda kuangalia mpira wa mechi ya ligi kuu kati ya Real Madrid C.F na F.C Barcelona iliyochezwa jana usiku Novemba 21, 2015.
Pia anatuhumiwa kuwa alikuwa amekunywa pombe hali ambayo inadhaniwa kusababisha kushindwa kufanya kazi na kutoa majibu yasiyoridhisha kwa wagonjwa.
Hata hivyo mganga huyo wa zamu amekutwa na Mkuu wa wilaya akiwa amelala, huku akikana tuhuma za kuwa alikuwa amekwenda kuangalia mechi ya mpira.
- Imenukuliwa kutoka FikraPevu
Post a Comment