Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Rais Magufuli kiboko aiseeeee .... afuta sherehe za uhuru


   

sefue (2)Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue

KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue ametoa taarifa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli amefuta sherehe za uhuru mwaka huu na badala yake, Desemba 9 itakuwa siku ya usafi nchi nzima ili kuondokana na tatizo la kipindupindu linaoikabili nchi.

Balozi Ombeni ameongeza kuwa, wakuu wa mikoa na wilaya zote wajiandae kuandaa vifaa vya vya usafi kwa ajili ya shughuli hiyo.

“Rais Magufuli ataangalia bajeti iliyokuwa imeandaliwa kwa ajili ya sherehe hizo, kisha ataielekeza kwenye sekta au wizara  atakayoona inauhitaji ili zikasaidie kule.


“Haipendezi kusherehekea miaka 54 ya uhuru huku kipindupindu kikituua, hivyo usafi ni muhimu kwa ajili ya afya zetu,” alisema Balozi Ombeni.

Hayo yamejiri wakati Balozi Ombeni alipofanya ziara kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili kukagua mashine za MRI na zile za CT-Scan na vitanda vilivyonunuliwa kutokana na agizo la Rais Magufuli kuamuru pesa zilizokuwa zimeandaliwa kwa ajili ya bajeti ya sherehe za ufunguzi wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano, mjini Dodoma Alhamisi iliyopita zielekezwe Muhimbili kununua vitanda vya wagonjwa.

NA DENIS MTIMA/GPL


Kwa mujibu wa Sheria ya Sikukuu za Kitaifa (The Public Holidays Act, Cap 35) pamoja na Sheria zingine zinazompa mamlaka Rais kutangaza siku yoyote kuwa sikukuu au mapumziko, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameamua kuwa maadhimisho ya Sherehe za Uhuru na Jamhuri zitakazofanyika tarehe 9 Desemba, 2015, yatumike kwa kufanya kazi.



Kwamba maadhimisho ya Uhuru ya mwaka huu (2015) yatatumika kama kichocheo cha kujenga tabia ya kufanya kazi (Uhuru na Kazi) katika Taifa letu. Mheshimiwa Rais ameelekeza Watanzania wote siku hiyo waitumie kwa kufanya kazi mbalimbali kama vile, mashambani, maofisini, sokoni, viwandani na usafi wa miji yao katika kutimiza dhana ya Uhuru na Kazi kwa vitendo.



Aidha, kwa kuwa Sherehe za Uhuru na Jamhuri huendana na Maandalizi mbalimbali ambayo yanatumia fedha, kwa kuzingatia kuwa siku hiyo itaadhimishwa kwa kufanya kazi, fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe hiyo sasa zitumike kwa shughuli zingine za kijamii ikiwa ni pamoja na kupambana na maradhi hasa kipindupindu, kununulia dawa za hospitali, vitanda vya hospitali n.k. kadri kamati za maandalizi zitakavyoamua.



Ieleweke kuwa sherehe za Uhuru na Jamhuri ni muhimu katika kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa nchi yetu. Hivyo, sherehe hizi zitaendelea kuadhimishwa kila mwaka kama kawaida kuanzia mwaka 2016.



Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Download Our App

1 comments:

Huyu mh. ni noma kweli kwa mwendo huu hatuhitaji upinzani juu ya hilo hongera

Reply

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top