Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ray C aomba radhi kuhusu video ya utupu Instagram

MSANII mtajika Rehema Chalamila, almaarufu Ray C ameomba radhi kwa mashabiki na wafuasi wake kufuatia video iliyomwonyesha akicheza densi akiwa uchi wa mnyama kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram.
Jumanne Oktoba 10,2015 video ya wimbo Mama Nitilie iliwekwa kwenye akaunti yake rasmi ya Instagram (@rayc1982) lakini ikafutwa dakika chache baadaye.

Akiongea kwenye redio ya Clouds FM ya Tanzania, Ray C alikubali kuwa aliyekuwa akicheza densi akiwa uchi ni yeye lakini hakujua aliyeiposti kwa akaunti yake.
“Ni kweli kwamba video iliwekwa kwa akaunti yangu ya Instagram ila mimi mwenyewe sikuiweka,” alisema mkali huyo wa kibao Wanitafutia Nini.
Ray C alifichua kuwa video hiyo ilirekodiwa kwa matumizi ya kibinafsi ya mchumba wake. Pia alisema kuwa simu yake iliibwa na mtu ambaye anaamini ni mmoja kati ya marafiki zake na anakisia rafiki huyo ndiye aliiposti kwenye mtandao.
“Simu yangu ilipotea Jumatatu. Nina uhakika kuwa ni rafiki yangu ninayemjua vizuri aliweka video hiyo baada ya kuitoa kwa simu yangu.
Kwa kawaida akaunti yangu ya Instagram huwa wazi kwa sababu simu ni kifaa changu binafsi. Sijawahi kufikiria kwamba mtu yeyote anaweza kuniibia simu,” akaeleza Ray C.
Msanii huyo hakusita kusema kuwa mchumbva wake ndiye aliirekodi video hiyo kwa matumizi yao binafsi.
“Nimeripoti kwa kampuni ya huduma za simu Vodacom na wakazuia laini yangu.Vodacom imefuta video hiyo kutoka kwa akaunti yangu,” akaongeza.
Ray C aliomba msamaha kutoka kwa wafuasi wake na umma kwa jumla.
“Sina la kusema. Naomba radhi kwa mashabiki wangu na umma. Naomba wanielewe kama nilivyoeleza kisa hiki. Nimepiga ripoti kwa polisi.,” Ray C akasema.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top