Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CAG AANIKA HALI YA UKAGUZI WA MAHESABU ULIVYO NCHINI

 Naibu Mkazi Mkuu  wa Hesabu za Serikali , Idara  na Mashirika ya Umma,  Benjamin Mashauri, akizungumza na waandishi wa habari (hawako pichani) kuhusu  ukaguzi  kwa Serikali Kuu, Mashirika ya mma na Serikali za Mitaa kwa mwaka 2014/15, Dar es Salaam, jana. Kulia ni  Sarah Reubeni, Msemaji wa ofisi ya  Taifa ya Ukaguzi. 

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
OFISI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),imesema kuwa ukaguzi wa mwaka 2014/2015  kwa serikali kuu haujakamilika hivyo kutumia rasimu hiyo ni makosa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Naibu Mkaguzi wa Mashirika ya Umma, Benjamin Mashauri amesema kuwa taarifa ya mkaguzi inakamilika ni baada ya kuiwasilisha kwa Rais kwa mujibu wa katiba inatakiwa iwasilishwe mwishoni mwa machi mwaka huu.

Mashauri amesema kuwa taarifa zinatolewa baadhi ya  vyombo vya habari na kunukuu ripoti ya CAG  kwa mwaka wa fedha 2014/2015 ni batili  kutokana na taarifa hiyo haijakamilika na wananchi wanatakiwa kupuuza taarifa hizo.

Amesema rasmu hiyo inayotumika baadhi  vyombo vya habari wakati taarifa hiyo haijakamilika na kukamilika kwake ni mara ya kuwasilishwa kwa Rais na kupeleka katika bunge na hapo inakuwa imekamilika kwa kutumia kwa ajili ya wananchi juu ya fedha ya umma ilivyotumika.

"Kuendelea kutumia rasmu hiyo wakati haijakamilika ni kupotosha watanzania na kukiuka maadili ya kiutendaji na taaluma yake kwa kuwapa taarifa zisizo na uhakika"amesema Mashauri.

Amesema kuwa ofisi hiyo itaendelea na kutekeleza majukumu yake yote kwa kuzingatia misingi na uwazi na uwajibikaji usiokiuka taratibu za kisheria katika kukusanya na kutumia rasilimali za umma.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top