Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI PROFESA MBARAWA AMCHARUKIA MKANDARASI MKOREA

Waziri wa ujenzi Makame Mbarawa ametoa wiki moja kwa mkandarasi anayetengeneza barabara ya njia nne kutoka Sakina hadi Tengeru mkoani Arusha kuhakikisha anatoa mikataba kwa wafanyakazi wa kitanzania wanaofanya kazi bila mikataka na akishindwa kufanya hivyo serikali itafuta mkabata wake kumshitaki na kumfukuza nchini.

Waziri Makame Mbarawa ametoa kauli hiyo wakati akikagua ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa kumi na nne nukuta moja inayo jengwa na kampuni ya Hanil-Jiangsu kutoka nchini Korea ambapo alipata malalamiko ya wafanyakazi wa kitanzania kufanyishwa kazi bila mikataba huku wakipata manyayaso kutoka kwa mkandarasi huyo.
 
Meneja wa wakala wa barabara mkoa wa Arusha John Kalupale amesema ujenzi wa barabara hiyo unakabiliwa na changamoto nyingi zilizosababisha kuchelewa kwa utekelezaji wake kwani hadi sasa ni asilimia saba tu ya ujenzi uliyofanyika na imebaki miezi tisa muda uliyo pangwa kumaliza.
 
Meneja wa miradi kutoka Tanrods makao makuu Mhandisi Deusidedit Kakoko amesema katika shilingi bilioni ishirini za kulipa fidia kwa watu wanaondolewa kupisha ujenzi huo tayari bilioni nne zimeshapatikana na hakuna mtu atayeondoshwa kwenye eneo lake bila kulipwa fidia.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top