Mtoto mdogo mwenye umri wa miaka minne aishie mtaa wa kazima katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi amechomwa moto kwenye mkono wake na baba yake mzazi baada ya kumtuhumu kuiba mboga aina ya chainizi.
Mtoto huyo ajulikanae kwa jina la George Noel amefanyiwa ukatili huo na baba yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Noel, ambaye kwa sasa anashikiriwa na jeshi la Polisi kwa tukio hilo la unyanyasaji.
Channel ten ilifika katika hospiotali ya wilaya ya Mpanda alikolazwa mtoto huyo kwa matibabu ambako muuguzi wa zamu Bertha Saimoni akathibitisha kumpokea mtoto huyo aliyekuwa akikabiliwa na maumivu makali.
Loading...
Post a Comment