Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CCM yamjibu hivi Mjane wa Kapt. Komba kuhusu mafao ya mumewe

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Mjane wa Marehemu, Kapteni Komba, Bi. Salome Komba kufuatilia malipo ya mafao ya mumewe kwa uongozi wa kundi la Tanzania One Theatre (TOT) ambako ndiko alikokuwa akifanyia kazi.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rodrick Mpogolo, ametoa maelekezo hayo ikiwa ni siku moja tu baada ya Salome kukaririwa  akimuomba Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli aingilie kati kumsaidia ili alipwe mafao ya marehemu mume wake yanayofikia Shilingi Milioni 75.

Mpogolo amesema ofisi yao haiwezi kulizungumzia suala hilo kwa sababu masuala yanayohusu fedha yanapaswa kufafanuliwa vyema na uongozi wa kundi lao la TOT ambako Komba alikuwa akifanya kazi.

“Ofisi yao haiwezi kulizungumzia kwa sababu masuala yanayohusu fedha yanapaswa kufafanuliwa vyema na uongozi wa kundi lao la TOT ambako Komba alikuwa akifanya kazi,” amesema.

Kwa mujibu wa Bi. Salome, hadi sasa wakati mumewe akitimiza miaka miwili tangu afariki dunia, CCM imemlipa Shilingi Milioni 4.5 tu ikiwa ni sehemu ya malipo hayo huku akifuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio kupata kiasi kilichobaki cha Shilingi milioni 70.5 bila mafanikio.

Komba aliyezaliwa mwaka 1954, alifariki dunia Februari 28, 2015 na kuzikwa Mkoani Ruvuma ambako enzi za uhai wake alijizolea umaarufu mkubwa kutokana na umahiri wake katika kutunga na kuimba nyimbo mbalimbali za kwaya, hasa za kukipigia debe chama chake (CCM) wakati wa kampeni mbalimbali za uchaguzi.

----------------

Piga ndege wawili kwa jiwe moja, ambapo utapata OFFERS mbili za kutangaza


Mosi; Kwenye blog http://www.ndgshilatu.blogspot.com ambapo litaweka kwenye USO wa blog pamoja na kurushwa Mara kwa Mara kama post ya habari.


Pili; Kama haitoshi tangazo lako tutalitangaza pia kupitia akaunti za FaceBook na Twitter za Blog hii.


Kwa kutangaza nasi biashara ama huduma yako itawafikia zaidi ya Watazamaji 50,000+ na zaidi ya nchi 120+ wanaozitembelea Blog na akaunti  hizi kila siku.


Kutokana na hii ni wazi kuwa Tangazo lako litawafikia watu wengi zaidi Duniani ndani ya muda mfupi


Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia e-mail pbuyegu2@gmail.com


Offer hii itadumu kwa muda mfupi tu ila tangazo lako litawekwa hewani kwa muda wa mwezi mzima.


Changamkia fursa hii adimu uimarishe Biashara yako.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top