Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mbowe, Mkewe wang'ang'aniwa Mahakamani



Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yamfungulia kesi MBOWE na mkewe, Dkt. Lilian Mtei kwa kukwepa kodi ya Serikali

Mitihani inazidi kumkabili mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kumfungulia kesi yeye na mkewe, Dkt. Lilian Mtei.

Mbowe, mkewe Dkt. Mtui pamoja na Meneja wa Klabu ya Bilicanas, Steven Mlingo wameitwa mahakamani kupitia barua ya wito iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya ya Ilala.
Mahakama imefanya uamuzi huo baada ya TRA kueleza kuwa imeshindwa kuwapata ili kuwapa hati ya wito mahakamani huku kesi hiyo iliyofunguliwa mwaka jana ikiwa imeshatajwa mara nne mahakamani hapo.
Washtakiwa hao waliofunguliwa kesi namba 402 ya mwaka 2016, wanakabiliwa na mashtaka matatu ikiwa ni pamoja na kutotumia mashine ya kielektroniki ya EFD kutoa risiti, kinyume cha Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015, kutoa nyaraka za uongo na kushindwa kutekeleza masharti ya sheria tajwa.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kutenda makosa hayo mwezi Mei mwaka jana jijini Dar es Salaam.
Mke wa Mbowe, Dkt. Mtei ni daktari anayefanya kazi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini mwanasheria wa TRA, Marcel Busegano aliieleza mahakama hiyo kuwa walifika hospitalini hapo kumpa barua ya wito bila mafanikio.

Awali, Mbowe aliburuzana mahakamani na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) iliyokuwa ikieleza kuwa inamdai zaidi ya shilingi bilioni 1 ya kodi ya pango iliyokuwepo club ya Billicanas, sakata lililopelekea club hiyo ya usiku kubomolewa.

----------------

Piga ndege wawili kwa jiwe moja, ambapo utapata OFFERS mbili za kutangaza


Mosi; Kwenye blog http://www.ndgshilatu.blogspot.com ambapo litaweka kwenye USO wa blog pamoja na kurushwa Mara kwa Mara kama post ya habari.


Pili; Kama haitoshi tangazo lako tutalitangaza pia kupitia akaunti za FaceBook na Twitter za Blog hii.


Kwa kutangaza nasi biashara ama huduma yako itawafikia zaidi ya Watazamaji 50,000+ na zaidi ya nchi 120+ wanaozitembelea Blog na akaunti  hizi kila siku.


Kutokana na hii ni wazi kuwa Tangazo lako litawafikia watu wengi zaidi Duniani ndani ya muda mfupi


Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia e-mail pbuyegu2@gmail.com


Offer hii itadumu kwa muda mfupi tu ila tangazo lako litawekwa hewani kwa muda wa mwezi mzima.


Changamkia fursa hii adimu uimarishe Biashara yako.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top