Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Serikali yawaita Waalimu Machi 16

Rais wa CWT, Gratian Mukoba 

Dar es Salaam. Siku moja baada ya walimu kuanza mgogoro na Serikali, Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kimepokea wito wa viongozi wake kukutana na Serikali Machi 16 kuzungumzia madai hayo.

Walimu walianza mgogoro wa kutokuelewana na Serikali wakishinikiza kulipwa madai yao yanayofikia takriban Sh800 bilioni.

Februari 7, CWT ilitoa siku 21 kwa Serikali kulipa madai ya walimu vinginevyo ingeanzisha mgogoro bila kutoa notisi nyingine.

Akizungumza jana, Rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema wamepata wito juzi wa kukutana na Serikali Machi 16 mjini Dodoma.

‘‘Licha ya wito huo, tunaendelea na mgogoro ulioanza leo (jana) hadi tutakapolipwa madai yetu, tutakapokutana na Serikali kama tutalipwa tutaacha, tusipolipwa tutaendelea nao,’ ’alisema Mukoba na kuongeza:

‘‘Tunaweza kutangaza kufanya maandamano kuuelezea ulimwengu kuhusu madai yetu, au tukaamua kukaa bila kufanya kazi.’’

Aliwataka walimu kuendelea na kazi hadi watakapotangaziwa hatua nyingine za kuchukua.

Mgogoro huo umeungwa mkono na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), ambalo limekitaka chama hicho kuendelea na mchakato wa kudai haki za walimu.

Rais wa shirikisho hilo, Tumaini Nyamhokwa alisema juzi kuwa Serikali imekuwa haitoi matumaini kwa walimu.

Madai ya walimu

Mukoba alisema walimu wanadai zaidi ya Sh300 bilioni, ambazo ni kwa ajili ya kuwalipa stahiki zao na kupandishwa madaraja.

Alisema walimu 80,000 waliopandishwa madaraja kati ya Januari na Aprili mwaka 2016, hawajarekebishiwa mishahara yao.

Madai mengine ni Sh480 bilioni za walimu wastaafu 6,044, wanaodai fedha zao tangu mwaka 2012.

Pia, kuna walimu 39,000 walio paswa kupandishwa madaraja mwaka huu wa fedha kuanzia Julai 2016 lakini hawajapandishwa hadi sasa.

Tayari, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo amenukuliwa akisema uhakiki wa deni la Sh10 bilioni umekamilika hivyo wanaendelea na mchakato wa ulipaji.

----------------

Piga ndege wawili kwa jiwe moja, ambapo utapata OFFERS mbili za kutangaza


Mosi; Kwenye blog http://www.ndgshilatu.blogspot.com ambapo litaweka kwenye USO wa blog pamoja na kurushwa Mara kwa Mara kama post ya habari.


Pili; Kama haitoshi tangazo lako tutalitangaza pia kupitia akaunti za FaceBook na Twitter za Blog hii.


Kwa kutangaza nasi biashara ama huduma yako itawafikia zaidi ya Watazamaji 50,000+ na zaidi ya nchi 120+ wanaozitembelea Blog na akaunti  hizi kila siku.


Kutokana na hii ni wazi kuwa Tangazo lako litawafikia watu wengi zaidi Duniani ndani ya muda mfupi


Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia e-mail pbuyegu2@gmail.com


Offer hii itadumu kwa muda mfupi tu ila tangazo lako litawekwa hewani kwa muda wa mwezi mzima.



Changamkia fursa hii adimu uimarishe Biashara yako.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana