Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kangi Lugola Kaanza na Sakata la Lugumi

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mh. Kangi Lugola ameweka wazi kwamba tayari amekwishampa taarifa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Simon Sirro kumuandalia taarifa muhimu kuhusiana na suala la Lugumi.
Mh. Lugola ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Mbeya ikiwa ni siku mbili tu zimepita tangu ale kiapo cha kuwa Waziri katika Wizara hiyo na kupokea maagizo hayo kama sehemu muhimu ya kuanzia kazi yake.

Kangi amesema kwamba amemuagiza Mkuu wa Polisi Simon Sirro kumuandalia taarifa itakayompa muongozo kushughulika na suala la Lugumi jambo ambalo Rais Magufuli amekuwa akitaka kupatiwa majibu haraka iwezekanavyo.

Aidha, Mh. Lugola amesema ingawa yeye siyo mgeni sana katika suala sakata hilo la Lugumi kwa kuwa jambo ameshalisikia mara kadhaa ndani ya bunge, ila sasa hivi anataka kulifuatilia jambo hilo kiofisi zaidi kuliko bungeni.

"Leo nimeanza na Mbeya, nimemuagiza Sirro juu ya kuniandalia taarifa itakayoniondolea ugeni katika suala la Lugumi. Lugumi siyo ngeni sana kwangu kwa kuwa mimi ni Mbunger na jmabo hili lilishakuja bungeni. Nataka kushughulika nayo kiosisi. Nikirudi Dar esa salaam sasa ndio nitadili na yale maagizo mengine kwa hiyo nao wanapaswa kukaa mkao" Lugola.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top