Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SHARO MILLIONEA OOH MAMA! AMEFARIKI DUNIA

 

Msanii aliyekuja juu kwa kasi kwa muziki na pia matangazo ya biashara likiwemo la Airtel Money la kampuni ya simu ya Airtel aliyejulikana kwa jina la Sharobaro a.k.a Sharo Milionea amefariki dunia leo.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Afande Constatine Masawe, amethibitisha  kutokea kwa  kifo cha  wa Sharobaro, kufuatia  ajali ya gari  katika kijiji cha Lusanga, Muheza, mkoani Tanga  ambako ndio nyumbani kwao.
 

Gari la Sharo Milionea alilopata nalo ajali
KWA MUJIBU WA WASANII WENZAKE AMBAO NI MWANADADA SHILOLE NA STEVE NYERERE (KWA WAKATI TOFAUTI),WAMETHIBIBISHA KUTOKEA KWA AJALI HIYO NA KUSEMA KUWA MSANII MWENZAO HUYO,AMEFARIKI DUNIA BAADA YA KUPATA AJALI HIYO,JIONI YA LEO.
 
Habari zaidi zitakuja kadri zitavyotufikia.
Globu ya Jamii imepokea habari hizi kwa mstuko na masikitiko makubwa kwani nyota ya Sharo Milionea ndiyo ilikuwa inaanza kung'ara katika anga za muziki pamoja na matangazo ya biashara, akiwa kayapumulia pumzi mpya wa ubunifu na weledi katika kupeleka ujumbe kwa watazamaji ambao wakubwa na wadogo walimpenda.
 
Mola aiweke roho ya marehemu 
mahali pema peponi - Amina
............................ Endelea kufuatilia NDGSHILATU BLOG nitakujuza zaidi ............

Download Our App

1 comments:

kwa kweli mimi ni mama ambaye si mshabiki sana na mambo ya miziki lakini kijana huyu ameniuma sana tena sana, na nimeanza kumfahamu kipindi kifupi sana hasa kwa kupitia matangazo ya Airtel na Azam kabla ya hapo sikuwa namjua kabisa. Mungu amlaze mahali pema peponi Amin.





Reply

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top