Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAZOEZI YA CUTLASS EXPRESS 2 KUANZA


Ofisa wa utendaji na Mafunzo wa Jeshi la Wanamaji wa Tanzanai Brigedia Jenerali Abdallah Athuman Mwemnjudi (kushoto) akitoa maelezo jana (leo) jijini Dar es salaam kuhusu kuanza kwa zoezi liitwalo Cutlass Express 2 linaloshirikisha wanamaji kutoka Marekani, Msumbiji, Netherland na Tanzania likiwa na lengo la kubadilishana uzoefu na mawazo juu ya kupambana na uharamia katika mwambao wa Bahari ya Hindi. Kulia ni Kiongozi wa Kundi namba 1 la wanamaji wa NATO Commodore Ben Bekkering.

                                                                     *********************
Na Tiganya Vincent-MAELEZO_Dar es salaam
Wanamaji kutoka nchi nne wameanza mazoezi nchini Tanzania kwa ajili ya kubadilishana mbinu za kukabiliana na maharamia katika mwambao wa Bahari ya Hindi. Madhumuni ya mafunzo hayo yanaendeshwa jijini Dar es salaam ni kubadilisha uzoefu , elimu na mbinu za kukabiliana na vitendo vya kiharamia ambavyo vimekuwa vikifanyika katika mwambao wa Bahari ya Hindi vya utekaji wa Meli mbalimbali zikiwemo za mizigo . Kauli hiyo ilitolewa jana (leo) jijini Dar es salaam na Brigedia Jenerali Abdallah Athuman Mwemnjudi wakati akitoa ufafanunuzi kwa waandishi wa habari juu ya zoezi hilo la pamoja linalozishirikiasha nchi mbalimbali lijulikanalo kama Cutlass Express 2. Alisema kuwa zoezi hilo linalowashirikisha Wanamaji wa Jeshi la Marekani, Msumbiji, Netherland na mwenyeji Tanzania litasaidia kuimarisha mapambano dhidi ya Maharamia kwa kubadilisha uzoefu na kupeana taarifa ambazo zitawezesha Maharamia kukamatwa kirahisi. Brigedia Jenerali Mwemnjudi alisema kuwa mafunzo watakayopata wanamaji wa pande zote yatasaidia katika kuwajengea uwezo wa kukabiliana na Mahamari katika hali yoyote na kuwana mbinu za Kimataifa za kukabiliana na Uharamia. Alisema kuwa lengo ni kuhakikisha kuwa suala ya uharimia katika Mwambao wa Bahari ya Hindi kutoa Pembe ya Afrika hadi Msumbiji ni salama kwa vyombo vyote vya majini na pia haitumiki kama njia ya biashara haramu kama vile uvuvi haramu, usafirishaji wa binadamu, na usafirishaji wa dawa za kulevya. Kuhusu hali ya Uharamia katika ukanda wa Afrika Mashariki Brigedia Jenerali Mwemnjudi alisema kuwa hivi sasa matukio yameanza kupungua ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo alitoa mfano kutoka mwaka 2010 hadi mwanzani mwa mwaka huu kulikuwa na matukio zaidi ya 30 ya uharamia ambapo maharamia 19 walikamatwa. Alisema kuwa kwa kipindi cha mwaka 2012 ni tukio moja lilitokea ambapo ni maharamia 12 walikamatwa. Brigedia Jenerali Mwemnjudi alisema kuwa mara nyingi maharamia upenda kutenda uhalifu huo hasa kipindi cha miezi ya kuanzia miezi Oktoba hadi Desemba wakati eneo la Bahari ni shwari. Mafunzo hayo yanatarajiwa kufungwa siku ya Jumanne ya wiki ijayo jijini Dar es salaam.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top