Chocheeni kuni mbichi ugali
uive mnacho taka kitokee!! Alikeni mamluki wakija wangojee!! Ni sehemu tu ya
kiitiko cha wimbo mpya wa Mkali wa kughani mashairi Tanzania na Afrika
Mashariki, Mrisho Mpoto ambao ameupakua na unakwenda kwa jina chocheeni
kuni.
Akizungumza na Father
Kidevu Blog kwa njia ya mtandao kutoka nchini India ambako amekwenda kwa
shughuli maalum za kikazi Mpoto amesema kuwa wimbo huo tayari upo hewani katika
Audio na Video.
“Nyimbo hii tayari ipo
hewani katika mitandao ya kijamii, na video yake tangu juzi ulinza kusikika
duniani kote,’ alisema mpoto.
Mpoto anasema wimbo wake
huo amemshirikisha chipukizi Ditto kutoka nyumba ya kukuza vipaji ya THT ya
Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Aidha anasema wimbo huo
umefanyiwa kazi na Mwandaaji wa muziki Allani Mapigo.
Miongoni mwa mistari
il;iyopo katika wimbo huo wa Nguli huyo ni pamoja na
“watanzania mwendakwao siku
zote haogopi giza”
“acheni nirudi nyumbani
safari imenishinda, naurizenu ntarudisha”
“mtu anaitapiga nyongo yake
anailamba tena anaagaliwa?”
“nisawa na tawi kavu
linapoanguka watu wakapiga kelele…Ahyaaaah!!”
“Katika misimu mmne kwa
mwaka tuongeze msimu mwingine wa tano wa kijivusha”
“Raha ya jamvi siku zote ni
viraka viraka,na dungu linamficha mlinzi wa ndege wakati wa mvua
tuu”
“Eti oooh! Imenyesha juzi
juzi tu maji sio mengi nisubirini kule, ilishindikana vipi kuyapima maji kwa mti
““ndio mkwaambia watu wavuke?”
“Mjomba! Binadamu ni sawa
na ganda la kitabu mpaka umfungue maandishi ndio uweze
kumuelewa”
“Eti lililotokea mbali
tufanye limepirta na haliwezi kumzuru mwingine”
“inayotaka kunyesha huwa
haisubiri mawingu”
“mimi sidhani kama
kujiponya kwa mambo mazito kunahitaji cheti kilichogongwa muhuri wa m,oto au
mtaalam wa magonjwa ya akili”
Zaidi ya kutumia neon sahau
tu, unawaulizaje watu magogo ya nini wakati unasema kuna nyoka?
Mjomba wewe si uliwapaka
wanja…ngoja wao wakupake pilipili halafu kwenye kombolela iwe zamu yako
kuzinga”
Mrisho Mpoto aliyezaliwa
miaka 34 iliyopita na kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa juzi ni msanii wa muziki
wa dansi, filamu, mwongozaji, ngonjela, mshairi, na sanaa yangoma kutoka
nchini Tanzania.
Anafahamika sana kwa jina
lake la utani kama Mjomba au Mpoto. Pia, ametamba sana kwa nyimbo zake
zilizogusa hisia za watu kama Salam Zangu Mjomba na Nikipata Naulialiyoimba
na Banana Zorro.


Post a Comment