Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAMISRI WAITISHA MAANDANO KUPIGA MAMLAKA YA RAIS.

 


Rais wa Misri Mohamed Morsi akiwa na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Hilary ClintonRais wa Misri Mohamed Morsi na Hilary Clinton.

Wafuasi na wapinzani wa rais wa Misri Mohamed Morsi wameitisha maandamano makubwa leo Ijumaa baada ya kiongozi huyo kujipa madaraka makubwa ambayo wachambuzi wansema kuwa yanamfanya kuwa dikteta.

Safu ya vikundi huria na visivyo na mlengo, ikiwa ni pamoja na wanaharakati waliokuwa mstari wa mbele katika harakati zilizomwondosha madarakani kiongozi mkongwe wa taifa hilo.

Hosni Mubarak mapema mwaka jana, wamepanga kufanya maandamano katika bustani ya Tahrir jijini Cairo, eneo ambalo ni kitovu cha maandamano, kupinga hatua ya kiongozi huyo ambaye amebatizwa jina la farao mpya.

Wafuasi wa Morsi wakiongozwa na chama chenye nguvu cha Muslim Brotherhood wamekusanyika nje ya kasri ya rais Kaskazini mwa jiji la Cairo kuonesha kuunga mkono uamuzi wa rais huyo kujiongezea madaraka na kujiweka juu ya sheria za nchi hiyo.

Taarifa zinaeleza kuwa rais Morsi anatafakari kuhusu kuhutubia umma wa taifa la Misri baadye hii leo kwa lengo la kutetea uamuzi wake.

Siku ya Alhamisi, rais alidhoofisha uwezo wa mahakama ambayo imekuwa ikifikiria kuweka usawa katika jopo linalotawaliwa na chama hicho cha kiislam kwa kutengeneza katiba mpya, kwa kuwaondolea majaji haki na mamlaka ya kuhoji kuhusu maamuzi yake.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top