Warembo mbalimbali wanaoishi 
Ulaya na walioshinda katika mashindano ya Miss East Africa huko Ulaya pia 
watashiriki katika mashindano ya Miss East Africa 2012 yatakayofanyika tarehe 
07 December katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam warembo 
hao ni:
1. MISS EAST AFRICA BELGIUM- Cynthia 
Ikwene (24)
2.MISS EAST AFRICA NETHERLANDS- Mareg 
Marcos (21)
3.MISS EAST AFRICA FRANCE- Fiona 
Ruboneka (24)
Fainali za mashindano ya Miss 
East Africa 2012 zitashirikisha warembo kutoka Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, 
Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, 
Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.
Mashindano ya Mwaka huu 
yanayosubiliwa kwa hamu yanatarajiwa kushuhudiwa na mamilioni ya watu Duniani 
kupitia kwenye luninga zao na pia kwa njia ya Internet ambapo yatautangaza 
utalii wa Tanzania kwa kiasi kikubwa na pia kujenga umoja wa Afrika mashariki na 
kudumisha utamaduni wa ukanda huu wa Afrika.
Mashindano ya Miss East Africa 
yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es 
salaam.
MISS EAST AFRICA NETHERLANDS- Mareg 
Marcos (21)

 




 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment