Waziri Mkuu Mizengo Pinda
akijibu maswali ya papo kwa hapo Bungeni mjinni Dodoma
leo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu wakitoka kwenye ukumbi
wa Bunge Mjini Dodoma, Novemba 1, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
**************************
Amani na utulivu uliopo
hapa nchini Tanzania utazidi kudumishwa daima ikibidi kwa njia yeyote na
watanzania wawe na amni na kufanya kazi zao bila kuwa na wasiwasi
wowote.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
aliwahakikishia watanzania leo wakati akijibu maswali ya wabunge mjini Dodoma
katika kikao cha tatu la Bunge la Kumi kinachoendelea mjini
Dodoma.
Pinda amesema kuwa kama
kuna mtu anadhani kuwa kwa kuleta chokochoko yake ataondoa amani na utulivu
uliopo hapa nchini Tanzania, basi mtu huyu anajisumbua na hayuko sahihi hata
kidogo.
Amesema kuwa ni kweli
kuna baadhi ya watu wengine wanajipatia kipato kwa kutaka kiuanzisha fujo za
kidini, watu wa aina hiyo tunawajua kwa sura na majina yao. Waziri ameahidi
kuwachuklia hatua kali za kisheria na kuwafikisha
mahakamani.




Post a Comment