Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Balozi Idd awataka wasamaria wema kujitokeza kuzisaidia hospitali kukabiliana na changamoto.


 

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akijiandaa kukabidhi msaada wa Vitanda 38 pamoja na Magodoro na Mashuka yake kwa Hoapitali Kuu ya Mnazi Mmoja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwajulia hali watoto waliolazwa kupatiwa huduma katika wodi ya ajali Mnazi Mmoja kabla ya kukabidhi msaada kwa ajili ya wodi hiyo.
Balozi Seif akimkabidhi Muuguzi Mkunga wa Wodi ya Watoto waliopata ajali Bibi Leluu Omar Said msaada wa vitanda 14, magodoro na mashuka kwa ajili ya wodi hiyo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akifuatana na Waziri wa Afya Mh. Juma Duni Haji, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Saleh Mohd Jidawi na Waziri wa Kazi, Uwezeshaji Wananachi Kiuchumi na Ushirika Mh. Haroun Ali Suleiman wakiangalia msaada wa vitanda, magodoro na mashuka yaliyotolewa na msamaria mwema katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akimpa pole mmoja wa wagonjwa wa wodi ya Mifupa aliyelazwa kabla ya kukabidhi msaada wa vifaa vilivyotolewa na wasamaria wema.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akimkabidhi Muuguzi dhama wa wodi ya Mifupa Bibi Afsa Abdulla msaada wa vitanda 24, magodoro na mashuka kwa ajili ya wodi hiyo.
Wafadhili na washirika wa Maendeleo wameendelea kukumbushwa kuchangia huduma za afya kwa nia ya kuwaondoshea mzigo wananachi pamoja na Serikali katika upatikanaji wa huduma hiyo muhimu.
Kumbusho hilo limetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, wakati akikabidhi Msaada wa Vitanda 28 pamoja na Magodoro, Mito na mashuka kwa ajili ya Wagonjwa wanaolazwa katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja.
Msaada huo wa Vitanda unaokadiriwa kugharimu shilingi za Kitanzania Milioni 12,000,000/- unazihusu wodi ya Watoto wanaopata ajali, Wodi ya Mifupa ya wagonjwa wa Kiume pamoja na chumba wanacholazwa wagonjwa wanaotumikia chuo cha mafunzo katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja.
Akikabidhi msaada huo uliotolewa na Wasamaria wema, Balozi Seif amesema bado Hospitali pamoja na Vituo vya afya hapa Nchini vinahitaji kupatiwa misaada ili viweze kutoa huduma katika kiwango kinachokubalika.
Amesema Serikali kwa upande wake itaendelea kujitahidi zaidi katika kutafuta wafadhili sambamba na kuongeza nguvu za upatikanaji wa vifaa vya huduma, lengo likiwa ni kuimarisha huduma za afya mijini na Vijijini.
Msaada huo unafuatia ziara ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliyoifanya katika sekta ya afya mwaka uliopita na kushuhudia changamoto kadhaa zinazovikabili vituo vingi vya afya, pamoja na Hospitali ukiwemo uhaba na uchakavu wa vitanda na magodoro ya wagonjwa.

Wakipokea msaada huo kwa nyakati tofauti Muuguzi Mkunga katika wodi ya Watoto Bibi Leluu Omar Said na Muuguzi dhamana katika Wodi ya Mifupa ya Wagonjwa wa Kiume Bibi Afsa Abdulla, wamewashukuru wafadhili hao kupitia Balozi Seif kwa msaada wao utakaosaidia kupunguza matatizo yanayozikabili hospitali hiyo.
Wauguzi hao wakuu wa wodi hizo wameahidi kwa pamoja kuvitunza Vifaa hivyo ili vidumu kwa muda mrefu kwa vile changamoto hiyo lilikuwa kilio chao cha muda mrefu.
Hata hivyo wauguzi hao wameiomba serikali kufanya utaratibu wa hifadhi zaidi ya magodoro hayo ili yadumu zaidi suala ambalo Balozi Seif ameuagiza Uongozi wa Wizara ya Afya kulifanyia kazi mara moja.
Mapema Balozi Seif alipata fursa ya kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika wodi zilizofanikiwa kupata msaada wa Vitanda, magodoro pamoja na Mashuka.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi anatarajiwa kutoa msaada kama huo hivi karibuni katika Hospitali za Micheweni na Vitongoji Kisiwani Pemba.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top