Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha
Kilelema kilichopo kwenye Wilaya Mpya ya Buhigwe,Mkoani Kigoma wakati wa Ziara
yake ya kutembelea maeneo hayo na kuweza kujionea changamoto mbali mbali
wanazokabiliana nazo wananchi hao ikiwa ni pamoja na kutembelea eneo
lililotengwa kwa ajili ya Ujenzi wa Soko la Kimataifa litakalowanufaisha wakazi
wengi wa wilaya hiyo ambao wako kando kando ya Mto Maragarasi unaopakana na nchi
jirani ya Burundi.Dkt. Migiro pia amewaasa wananchi wa maeneo hayo kuwa na
umoja,mshikamano na upendo ili kuweza kuhimarisha mambo mbali mbali ya
Wilaya.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akihutubia Mkutano wa hadhara kwenye
Kijiji cha Buhigwe ambapo ndipo yalipo makao makuu ya Wilaya Mpya ya
Buhigwe,Mkoani Kigoma wakati wa Ziara yake ya kutembelea wilaya hiyo
jana.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akicheza ngoma ya asili ya kabila la
Waha waliokuja kumpokea.
Wananchi wa Kijiji cha
Buhigwe wakimuaga Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose
Migiro.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akisalimiana na Viongozi mbali mbali
wa CCM katika Kijiji cha Mnanila,Wilayani Buhigwe.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwasalimia wananchi wa Kijiji cha
Mnanila kilichopo kwenye Wilaya Mpya ya Buhigwe,Mkoani Kigoma wakati akiendelea
na Ziara yake ya kutembelea Kata zote zilizopo wilayani humo.
kwa picha zaidi bofya read more
kwa picha zaidi bofya read more
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akizungumza na wananchi wa Kijiji
cha Buhigwe ambapo ndipo yalipo makao makuu ya Wilaya Mpya ya Buhigwe,Mkoani
Kigoma wakati wa Ziara yake ya kutembelea wilaya hiyo jana.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwapungia watoto wa Kijiji cha
Kilelema kilichopo kwenye Wilaya Mpya ya Buhigwe,Mkoani Kigoma mara baada ya
kumaliza kuwahutubia wananchi wa Kijiji hicho jana.
Mmoja wa wananchi wa
Kijiji cha Buhigwe ambapo ndipo yalipo makao makuu ya Wilaya Mpya ya
Buhigwe,Mkoani Kigoma wakati wakimsikiliza Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa
Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro aliekuwa kwenye Ziara ya kutembelea wilaya hiyo
jana.
Mkuu wa Wilaya ya
Buhigwe,Ndg. Gishuli Mbegesi (kulia) akikabidhi Taarifa ya Utekelezani wa Ilani
ya Uchaguzi kwa Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose
Migiro.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akipokea ripoti ya Chama Wilaya ya
Buhigwe,kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Buhigwe,Bi. Bennosa Mjema.Katikati ni
Mwenyekiti wa CCM Wilaya hiyo,Ndg. Elisha Bagwanya
Baadhi ya Wakazi wa
Kijiji cha Buhigwe wakimsikiliza Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa
Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro aliekuwa kwenye Ziara ya kutembelea wilaya hiyo
jana.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akicheza ngoma ya asili ya kabila la
Waha sambamba na Bibi Buchiro Edmas Kapina wakati wa Ziara ya kutembelea wilaya
ya Buhigwe,Mkoani Kigoma jana.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akilakiwa kwa shangwe na kinamama wa
Kijiji cha Kilelema.
Mjumbe wa Halmashauri ya
Kijiji cha Kilelema,Everist Samson akisoma taarifa ya kijiji kuhusiana na
changamoto mbali mbali zinazowakabili wananchi wa kijiji hizo zikiwemo zile za
kuvamiwa na majambazi wanaotoka nchi jirani ya Burundi.Kijiji hiki kipo mpakani
kabisa mwa Tanzania na Burundi kwa kijiji cha Buhema Mkoani Lutana,nchini
Burundi.
Wananchi wa Kijiji cha
Kilelema kilichopo kwenye Wilaya Mpya ya Buhigwe,Mkoani Kigoma wakimsikiliza kwa
makini Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro
(hayupo pichani).
Mwenyekiti wa Kijiji cha
Kilelema,Benedict Samson Mahuta (kulia) akitoa ufafanuzi juu ya eneo la Soko kwa
Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro
(katikati),alietembelea eneo litakalojengwa soko la Kimataifa katika Kijiji
hicho cha Kilelema.
Picha ya Pamoja na
Watendaji wa Kijiji cha Kilelema.
Katibu wa NEC,Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro (pili kulia) akiongozwa na Mkuu wa
Wilaya ya Buhigwe,Ndg. Gishuli Mbegesi Charles (kushoto) kuelekea kwenye eneo la
mpaka wa Tanzania na Burundi unaotenganishwa na sehemu ya Mto
Maragarasi.
Post a Comment