Mwenyekiti wa CCM
mkoa wa Singida, Mgana Izumbe Msindai akihutubia kwenye mkutano wa hadhara
uliofanyika kwenye kituo cha zamani cha mabasi mjini Singida, Msindai alikuwa
akijitambulisha kuvunja makundi na kupokea kero mbalimbali za
wananchi.
Baadhi ya wanaccm
na wananchi wa Singida mjini wakimsikiliza kwa makini mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Singida, Mgana Izumbe Msindai (hayupo kwenye picha) wakati akihutubia.(Picha na
Nathaniel Limu).
Na Nathaniel
Limu.
Wanachama wa Chama
Cha Mapinduzi (CCM) na wananchi wa mkoa wa Singida kwa ujumla, wameaswa
kutumia mwaka huu mpya, kujiwekea malengo ya kufanya kazi halali kwa bidii
na maarifa ili waweze kujiletea maendeleo makubwa zaidi kuliko yaliyopatikana
mwaka jana.
Changamoto hiyo
imetolewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa Singida Mgana Izumbe Msindai, wakati
akiutubia wananchi wa Manispaa ya Singida kwenye kwenye mkutano wa hadhara
uliofanyika katika kituo kikuu cha mabasi cha zamani
mjiniSingida.
Amesema kujituma
kufanya kazi kwa bidii, maarifa na kwa malengo, ndio njia pekee inayoweza
kumsaidia mwananchi ye yote kujikomboa kiuchumi na kupelekea kuishi maisha
bora.
Akifafanua zaidi,
Msindai amesema linapokuja suala la maendeleo, ni lazima itikadi za kisiasa
ziwekwe pembeni, ili maendeleo endelevu ya mtu mmoja mmoja, wilaya, mkoa na hata
taifa, yaweze kupatikana.
Msindai ambaye ni
maarufu kwa jina la CRDB benki inayomjali mteja, ametumia fursa hiyo kuwashukuru
wana CCM kwa kumchagua kwa kishindo kushika nafasi ya mwenyekiti CCM
Mkoa.
Wakati huo huo,
Msindai amesema kuwa wamekubaliana na manispaa ya Singida, kituo kikuu cha
zamani cha mabasi, kuanzia sasa kitumike kwa mabasi madogo kushusha abiria hadi
hapo manispaa itakapoanza kujenga kitega
uchumi.




Post a Comment