Jeshi
la Polisi mkoa wa Arusha limefanikiwa kukusanya kiasi cha Bilioni 1.2 kwa mwaka
2012 ambapo mwaka jana jeshi hilo lilikusanya zaidi ya Milioni 518 kutokana
na makosa mbalimbali ambayo yanatozwa mara baada ya wananchi kuvunja sheria za
Jeshi hilo
Akiongea na “FULL
SHANGWE”jana kuhusuniana na mapato ya jeshi hilo kwa mkoa wa Arusha kamanda wa
polisi mkoani hapa Liberatus Sabas alisema kuwa kuongezeka kwa fedha hizo
kunatokana na jitihada mbalimbali za jeshi hilo za kupambana na
uhalifu.
Sabas alisema kuwa mbali
na jeshi hilo kuweza kupambana na uhalifu hivyo kukusanya kiwango kikubwa sana
cha fedha lakini hata uhalifu wenyewe, ajali za barabarani nazo zimepungua
tofauti na miaka ya nyuma kutokana na jitiada ambazo zinafanywa na
Polisi
Aliongeza kuwa kwa kipindi
cha mwaka 2011 matukio ya ajali za barabarani yalikuwa ni 2507 wakati mwaka 2012
matukio yatokanayo na ajali yalikuwa ni 2106 sawa na upungugu wa asilimia
16
Akiendelea kuelezea pia
alisema kuwa hata matukio ya vifo vitokanavyo na ajali navyo vimepungua kwa
kiwango cha hali ya juu sana ambapo kwa mwaka 2011 matukio yalikuwa 211 huku
2012 yalikuwa ni 175 sawa na upungufu wa asilimia 17 ambapo hali hiyo imetokana
na Jitiada mbalimbali ambazo zinatokana na Jeshi hilo
Mbali na hayo pia makosa
ya barabarani ambayo yamelipiwa nayo yamechangia sana kuinua pato letu la mwaka
ambapo yalikuwa ni zaidi ya elfu 42 kwa mwaka 2012 tofauti na mwaka 2011 ambapo
makosa hayo yalikuwa ni 1978 sawa na ongezeko la makosa ya barababarani
yaliyolipiwa kwa asilimia 119
Kutokana na hali hiyo
Kamanda Sabas aliwataka wananchi wa Mkoa wa Arusha kuhakikisha kuwa wanakuwa
walindaji wazuri wa sheria za nchi na wala sio wavunjaji wazuri wa sheria za
Nchi kwani uvunjwaji wa sheria za nchi ndio chanzo cha vifo ,Umaskini pamoja na
Migogoro mikubwa sana ndani ya
jamii.
Post a Comment