Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Pius Makuru Nyambacha kuwa
Kamishna Jenerali wa Zimamoto na Uokoaji nchini.
Taarifa iliyotolewa mjini Dar Es Salaam na
kutiwa saini na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, Januari 30, 2013
inasema kuwa uteuzi wa Bwana Nyambacha ulianza Jumanne ya Januari 22, mwaka huu,
2013.
Aidha, taarifa hiyo inasema kuwa kabla ya uteuzi
wake, Bwana Nyambacha alikuwa Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji.
Post a Comment