CESC FABREGAS jana usiku aliingia kwenye orodha ya wafungaji katika mchezo wa raundi ya kwanza Kombe la Mfalme wakati alipofungia Barcelona bao la kuongoza katika dakika ya 50 kupitia pasi ya Lionel Messi.
Lakini beki kinda wa
kifaransa, Raphael Varane aliyeonyesha kiwango kikubwa, aliisawazishia Real
Madriad katika dakika ya 85.
Wafungaji wanaoongoza
katika timu hizo, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo walijikuta wakitoka uwanjani
bila goli.
Ronaldo alicheza vizuri
na ilikuwa ni bahati mbaya kwake kutoka mtupu.
Kiungo wa Barcelona,
Xavi aligonga mwamba katika hatua za mwanzo na pia alipiga shuti lililokolewa na
beki wa zamani wa Chelsea, Ricardo Carvalho kabla mpira haujaingia
wavuni.
Post a Comment