Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameweka wazi kuwa serikali yake inakusudia kujenga kujenga nyumba kwa ajili ya waalimu na madaktari katika maeneo yao ya kazi.
Akizungumza alipotembelea shule ya Sekondari ya Kazo iliypo wilaya ya Kiruhura rais huyo aliyekuwa ameambatana na mkewe, ameahidi kutoa msaada wa basi katika shule hiyo ya mchanganyiko.
Chini ya Mpango wa Elimu ya Sekondari kwa Wote, serikali imetumia jumla ya shilingi milioni 565 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 12 na maabara 2 za kisayansi katika shule hiyo.
Aidha asema kuwa serikali itajenga darasa la kompyuta na maktaba shuleni hapo.