Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Baadhi ya Viwanda na Mahoteli jijini Dar mbioni kufungiwa kwa uchafuzi wa mazingira


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mh. Dkt. Terezya Huviza akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika kiwanda cha bia cha Serengeti, ambapo amesema kutokana na hali alioiona pale, itabidi kwanza kuwashirikisha NEMC na kuona jinsi gani watashauriana na kama itabidi kukifunga itabidi aondoe hati ya mazingira kisha kukifunga kiwanda hicho.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mh. Dkt. Terezya Huviza leo ameendelea kufanya ziara za kushtukiza katika viwanda na mahoteli mbalimbali jijini Dar es salaam kuangalia hali ya usafi wa mazingira.

Katika ziara hiyo Mh waziri na ujumbe wake wametembelea kiwanda cha Bia cha Serengeti, CI Group Marketing Solution, Coco Beach, hoteli za Golden Tulip na Sea Cliff.

Akitoa maamuzi kuhusu mazingira aliyoyakuta katika kila sehemu, Mh. Dkt. Huviza amesema Kiwanda cha Serengeti kina mfereji unaomwaga maji machafu na bahati mbaya unatitirisha katika makazi ya watu kitu ambacho ni hatari, hivyo atashauriana na NEMC na Mwanasheria waone jinsi ya kuwasaidia, lakini kama itashindikana kwa kuwa maji wanayomwaga ni mengi sana itabidi wafunge kwa muda.

Kuhusu maeneo mengine aliyoyatembelea Mh. Waziri amesema hawezi kutoa maamuzi kwa sasa kwa sababu kila aliyekutwa na makosa amepewa muda wa kuyarekebisha na ambaye atashindwa kufanya hivyo basi atafungiwa kwa mujibu wa sheria.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Mh. Dkt Terezya Huvisa akiwasili katika kiwanda cha bia cha Serengeti Breweries baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika kiwanda hicho kujionea namna gani wanatunza Mazingira.




Afisa Mazingira wa Kiwanda cha Serengeti Breweries Dominick Elibariki akitoa maelezo ya namna wanavyotibu maji taka ya kiwanda hicho kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mh. Dkt. Terezya Huviza aliyeambatana na maafisa kutoka Baraza la Hifadhi ya Mazingira (NEMC).


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mh. Dkt. Terezya Huviza akiendelea na ukaguzi wa maeneo mbalimbali ya kiwanda hicho.


Moja ya mtaro unaotiririsha maji yenye kemikali yanayotoka ndani ya kiwanda cha Kampuni ya Serengeti Breweries uliolekezwa na kupitisha maji yake yenye harufu kali karibu na makazi ya watu.


Sehemu ya mtaro wa maji machafu yanayotoka ndani ya kiwanda cha bia cha Serengeti ambao umesafishwa na kulundika lundo la uchafu pembezoni mwa ukuta wa nyumba ambayo ni makazi ya watu.


Mkazi wa Kata ya Chamwenyewe iliyopo maeneo ya Chang’ombe Bi. Mwaka Washokera akimweleza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Mh. Dkt Terezya Huvisa adha anayoipata yeye na familia yake kutokana na mtaro wa maji machafu ya kampuni ya bia ya Serengeti ambao umepita uwani kwake, na kipindi cha mvua kusababisha maji machafu yenye kemikali kuingia katika nyumba yake.

Mama huyo pia amesema kampuni hiyo imemnyanyasa kijinsia kwani alikuwa akilima bustani ya Mboga uwani kwake lakini kutokana na mtaro huo kupita karibu na uani kwake ameshindwa kuendelea na bustani hiyo amelalamikia pamoja na moshi mzito unaotoka ndani ya kiwanda hicho na kusababisha watoto kukohoa kila mara.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Mh. Dkt Terezya Huvisa akiangalia mtaro wa maji machafu uliopita uani kwenye nyumba ya Mama Mwaka Washokera.


Afisa Mkuu wa Mazingira wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Bi. Ruth Lugwisha akichukua sampo ya maji yanayotiririka kutoka katika kiwanda cha Serengeti Breweries kwa ajili ya vipimo kama yana madhara kwa binadamu ambapo bomba lake limeelekezwa kwenye makazi ya watu.


Mtaro wa maji yenye kemikali unaotokea kwenye kiwanda cha CI Group cha uchapishaji kilichopo jirani na kiwanda cha bia cha Serengeti kilichopo maeneo ya Chang’ombe.


Mkazi wa Kata ya Chamwenyewe Bi. Mwamtema akimuonyesha Waziri wa Mazingira Dkt. Therezya Huvisa adha wanayoipata kutokana na maji yanayotiririka kutoka kwenye viwanda hivyo ambayo hujaa katika mifereji hiyo na kuingia katika makazi.


Mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda cha CI Group akimuonyesha Waziri Upande zilipo Ofisi za mabosi wa kampuni hiyo ambapo katika Mazingira ya kutatanisha walikuwa hawaonekani kiwanda hapo baada ya Waziri kuingia lakini cha kushangaza magari yao yalikuwa yamepaki nje ya ofisi hizo kuonyesha kwamba wapo ndani.


Pichani Juu na Chini ni sehemu ya kupunguza stress wanayotumia wafanyakazi wa kiwanda cha CI Group wakiwa wameandika ujumbe unaosemeka” Tumechoka na Vyoo” ambapo Mheshimiwa Waziri aliamua kuingia kukikagua na kujionea hali halisi.


Kumradhi kama picha hii itakukwaza lakini haya ndio mazingira ya kazi kwenye baadhi ya viwanda vyetu nchini.



Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho wakifurahia ujio wa Waziri wa Mazingira wakijua ya kwamba wataboreshewa mazingira ya kufanyia kazi.


Pichani Juu na Chini Waziri wa Mazingira Dkt. Therezya Huvisa akikagua mtaro wa maji machafu ya kiwanda hicho.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top