Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

JAMBO LEO BINGWA MPYA FAINALI ZA NSSF 2013

 


Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amosi Makala, akimkabidhi kombe la Ubingwa wa michuano ya NSSF Media Cup naodha wa timu ya Jambo Leo, Said Mwishehe, baada ya timu hiyo kuifunga Changamoto bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliochezwa leo asubuhi kwenye Uwanja wa TCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amosi Makala, akimkabidhi kombe la Ubingwa wa michuano ya NSSF Media Cup naodha wa timu ya Business Times 'Business Queens', Lulu Habibu, baada ya timu hiyo kuifunga TBC jumla ya mabao 39-18 katika mchezo wa fainali uliochezwa leo asubuhi kwenye Uwanja wa TCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam.

Mshambuliaji wa Jambo Leo, Julius Kihampa, akichuana kuwania mpira na beki wa Changamoto, Emmanuel Balele, wakati wa mchezo huo wa Fainali uliochezwa leo asubuhi kwenye Uwanja wa Tcc Chang'ombe. Katika mchezo huo Jambo Leo imeibuka na ushindi wa bao 1-0 na kutangazwa kutwaa kombe hilo la NSSF CUP 2013 na kuwa bingwa mpya wa michuano hiyo iliyomalizika leo.
Beki wa Jambo Leo, Mohamed Akida, akimdhibiti kiungo mshambuliaji wa Changamoto, Hamad Ganichiaga, wakati wa mchezo huo.
Beki wa Jambo Leo, Mohamed Akida, akiruka kuokoa moja ya hatari langoni kwake.
Kiungo Mshambuliaji wa Changamoto, Hamad Ganichiaga (kulia) akijaribu kumtoka beki wa Jambo Leo, Mansour Mohamed, wakati wa mchezo huo.
Beki wa Jambo Leo, Mansour Mohamed (kushoto) akimdhibiti Kiungo Mshambuliaji wa Changamoto, Hamad Ganichiaga, wakati wa mchezo huo.
Beki wa Changamoto, Emmanuel Ganichiaga, akichuana kuwania mpira na mshambuliaji wa Jambo Leo, Zahor Milanzi, wakati wa mchezo huo.
Kipa wa Jambo Leo, akiokoa moja ya hatari langoni mwake.
Julius Kihampa (chini) akicheza takorling....
Kina Dada wa Jambo Leo, wakiwahamasisha kaka zao.
Benchi la Ufundi la Changamoto na wachezaji wa akiba.
Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amosi Makala, akiwa meza kuu na baadhi ya viongozi wengine.
Benchi la Jambo Leo. NA SUFIANI MAFOTO
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top