Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUWA MFANO WA KUIGWA

 




Na Frank John - Maelezo
Watumishi wa umma wametakiwa kuwa mfano wa kuigwa katika kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa taaluma zao hasa katika kitengo cha manunuzi ili sekta binafsi ziweze kujifunza kutoka kwao.

Wito huo umetolewa jana na Kamishna wa Idara ya Manunuzi ya Umma kutoka wizara ya Fedha Dk. Fredrick Mwakibinga katika kongamano la kujadili rasimu ya sera ya manunuzi lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa JB uliopo jijini Dar es Salaam.

Dk Mwakibinga pia aliwataka Maafisa ugavi, wananchi na wadau mbalimbali kutoa maoni yao juu ya rasimu ya Sera ya manunuzi ya Umma ili waweze kufanikisha zoezi la mchakato wa uundwaji wa sera hiyo.

Alisema kuwa kupatikana kwa sera nzuri na ya kisasa ya manunuzi ya umma ambayo ni muongozo wa Serikali katika sekta hiyo, kutaisaidia Serikali kutimiza nia na malengo ya kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli.

“Tunayo mambo mengi ya kuangalia kama Serikali ili kuboresha sekta hii, ikiwa ni pamoja na kuangalia miundo ya Idara za ugavi, idadi ya watumishi na kuwajengea uwezo wagavi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi zaidi”, alisema Dk. Mwakibinga.

Alizitaja njia zitakazotumika katika utoaji wa maoni ili kuboresha rasimu hiyo kuwa ni baruapepe, nukushi, barua na kupitia vyombo vya habari kama magazeti ambapo mwananchi atachangia kitu anachohitaji kiwepo kwenye rasimu hiyo.

Alimalizia kwa kusema kuwa baadhi ya mambo ambayo Serikali inahitaji kuyaangalia ni minundo ya Idara za Ugavi, idadi ya watumishi na kuwajengea uwezo wagavi ili waweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
Akitoa mada katika kongamano hili Prof. Gaspar Munishi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala alisema kuwa kuna umuhimu wa kuboresha rasimu ya Sera ya manunuzi kwani inayotumika sasa ni ya zamani na haikidhi mahitaji yaliyopo.

Prof. Munishi pia alishauri kuwa ni lazima sera ya manunuzi iendane na sheria na taratibu za Serikali na uhusiano wa kimataifa kati yake na washirika wa maendeleo ili kuweza kutimiza sheria zilizopo.

Akichangia mada katika kongamano hilo Emmanuel Maliganya ambaye ni Afisa Ugavi kutoka Benki Kuu ya Tanzania, alitoa wito kwa wadau mbalimbali kulipa uzito jambo hilo na kuweza kutoa maoni yao ili yawezeshe kupatikana kwa sera bora.

Alitaka suala la rushwa liainishwe katika sera ya manunuzi ya umma ili wale wote wanaoshiriki katika vitendo vya rushwa ndani ya mchakato wa manunuzi ya Serikali bila afisa ugavi kuhusika, wawajibishwe.

Kongamano hilo la siku moja liliandaliwa na Idara ya Sera ya manunuzi ya umma na kuhudhuliwa na wajumbe mbalimbali kutoka ofisi za Serikali na Taasisi binafsi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top