Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Katibu Mkuu Wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta)Nicolaus Mgaya naye Chupuchupu kung’olewa Katibu Mkuu

 


Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta)
---
Dar es Salaam: Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), Ayoub Omar kuvuliwa wadhifa wake, imebainika kuwa Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Nicolaus Mgaya naye amenusurika kung’olewa kwenye wadhifa wake.

Mgaya aliliambia Mwananchi jana kuwa njama za kumng’oa kwenye wadhifa huo zilipangwa na wapinzani wake ambao walitoa hoja dhaifu bila ushahidi kuwa ana uhusiano wa wanawake (hawakutajwa).

“Hoja zao hazikuwa na maana, walikuwa wakihisi tu kuwa natembea na mwanamke fulani bila kuwa na ushahidi, pia suala hilo halihusiani na utendaji wangu wa kazi,” alisema Mgaya na kuongeza:


“Unajua katika umoja wowote lazima kuwe na majungu watu wanaweza kuwa na sababu zao nyingi tu, hivyo sikuona ajabu niliposikia nafanyiwa zengwe.”


Alisema hoja za kutakiwa kung’oka zilijadiliwa na kumalizwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji kilichomalizika juzi, ndiyo maana hazikuibuka tena katika kikao cha Baraza Kuu la Tucta kilichomalizika jana jioni. Kwa Habari zaidi Bofya na Endelea.......>>>>
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top