Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Kenya yatakiwa uchaguzi wa amani kudhidirisha ukomavu wa demokrasia

 


Wagombea wa uraisi nchini Kenya

Wakati harakati za kampeni za uchaguzi wa uraisi zinafikia ukingoni nchini Kenya, Marekani imewataka raia wa Kenya kufanya uchaguzi wa amani ili kumpata kiongozi mpya kwa amani.

Akizungumza kwa niaba ya serikali naibu msemaji wa serikali ya Marekani Patrick Ventrell ameongeza kuwa Kenya inapita katika kipindi cha muhimu na kihistoria na hivyo kuwasihi wagombea kuhakikisha wanaepuka kuwa sababisho la umwagaji damu kama uliowahi kutokea katika uchaguzi wa mwaka 2007.

Hata hivyo hali ya mvutano imeongezeka ambapo serikali ya Marekani imewataka wakenya kutumia fursa hiyo kudumisha ukomavu wa demokrasia na kutekeleza matakwa ya katiba mpya.

Msemaji huyo amesema kuwa ni matarajio ya wengi kuwa wakenya hawatajali jinsi,kabila,dini,eneo analotoka mgombea ili kuchagua bali bali watamchagua kiongozi bora kulingana na sifa stahiki.

Takribani raia elfu moja walipoteza maisha huku laki sita wakiyakimbia makazi yao katika machafuko yaliyotokea katika kipindi cha uchaguzi wa mwaka 2007.

Via kiswahili.rfi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top