Mkuu wa wilaya ya Morogoro Saidi Amanzi akipiga
mpira na kufunga bao la penalti ikiwa ni ishara ya ufunguzi rasmi wa mashindano
ya vyuo vya Utumishi wa umma Tanzania katika uwanja wa Jamhuri
Morogoro.
DC Amanzi akizungumza na wanamichezo muda mfupi
kabla ya mashindano hayo kuanza kutimua vumbi katika viwanja vya Jamhuri
Morogoro.
Mchezaji wa Tabora Sport
Club Maria Musiba kulia akitafuta mbinu ya kufunga huku mchezaji mwenzake Grace
Allan akijiandaa kutoa msaada dhidi ya wachezaji wa timu ya Magogoni Dar es
Salaam, Georgia Lugalinda na Matrida Swai wakati wa mchezo wa ufunguzi wa
mashindano ya vyuo vya utumishi wa umma Tanzania katika uwanja wa jamhuri
Morogoro ambapo katika mchezo huo Tabora ilishinda kwa vikapu 35-5 katika uwanja
wa ndani Jamhuri mkoani Morogoro.
KIKOSI CHA TIMU YA TABORA KILICHOIBUKA NA
USHINDI WA BAO 1-0 DHIDI YA MAGOGONI DAR ES SALAAM
KIKOSI CHA TIMU YA MAGOGONI DAR ES SALAAM
KILICHOPOKEA KIPIGO KUTOKA KWA TABORA KWA USHINDI WA BAO 1-0.
Mchezaji wa timu ya Singida akijaribu kuwatoka
wachezaji wa Magogoni Dar es Salaam katika mchezo wa basketiboli ambapo Singida
ilipoteza kwa vikapu 44-28
Post a Comment