Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CSSC yashinda Tuzo ya SADC kutambua mchango wa mashirika ya dini katika masuala ya jinsia

 


Bi. Rachel Mkundai akikabidhi Tuzo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa CSSC Bw. Peter Maduki.
Afisa uhusiano wa CSSC Bi. Rachel Mkundai akikabidhiwa Tuzo kutoka kwa waandaji “Gender Links”
--
Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC) imeshinda Tuzo ya kutambua mchango wa mashirika ya dini katika kuwawezesha wanawake kutambua haki ya afya ya uzazi. Tuzo hiyo imetolewa na Shirika linalotetea masuala ya jinsia (Gender links) ukanda wa nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) lenye makao yake makuu nchini Afrika Kusini.

CSSC ilitangazwa mshindi na kukabidhiwa Tuzo hiyo wakati wa kilele cha mkutano mkuu wa masula ya jinsia ya ukanda huo uliofanyika nchini Afrika ya Kusini.

Mashindano hayo yalihusisha washiriki 213 kutoka nchi 13 ambazo ni wanachama wa SADC, na CSSC iliibuka mshindi katika kupengele cha mashirika ya dini na kuwashinda wengine 13 katika kipengele hicho.

Ushindi wa CSSC umepatikana baada ya kuwasilisha makala ya filamu (Documentary) kuhusu namna ya kumsaidia mtoto aliyezaliwa kabla ya miezi tisa (Pre-mature) kukua na kuongezeka uzito unaostahili kwa kutumia njia ya asili maarufu kama “Kangaroo method” Njia hii inatumika katika hospitali ya wilaya ya Sengerema inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Geita.

Na
Renatus Sona
Afisa Habari -CSSC
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top