Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

HAWA GHASIA AAGIZA HALMASHAURI ZA WILAYA KUUNDA MABALAZA YA WAFANYAKAZI

 


waziri ghasiaNa Gladness Mushi wa Fullshangwe- Arusha
HALMASHAURI za wilaya nchini zimeagizwa kuunda mabaraza ya wafanyakazi ili kuweza kuyapatia ufumbuzi malalamiko ya wafanyakazi sehemu za kazi na kuboresha utendaji wenye kuleta tija..
 Waziri wanchi ofisi ya waziri mkuu Tawala za mikoa na serikali za mitaaa, TAMISEMI,Hawa Ghasia  ameyasema hayo jana  alipokuwa akifungua kikao cha siku mbili cha baraza jipya la majadiliano ya pamoja katika sekta ya serikali za mitaa nchini.
 Amesema baraza la majadiliano katika sekta ya serikali za mitaa lina jukumu kubwa la kuishauri serikali kuhusu masuala mbalimbali ya uendeshaji wa mamlaka za serikali za mitaa ,ikiwemo masuala ya utumishi,.mifumo,sheria, taratibu na miundo mbalimbali ya uendeshaji wa shughuli za mamlaka za serikali za mitaaa.
 Waziri Ghasia,amesema  halmashauri ambazo hazijaunda mabaraza hayo kuhakikisha zinayaunda, na yale ambayo yamemaliza muda wake wanachaguliwa wajumbe wapya na kuhakikisha mabaraza yote yanakaa vikao ili kuweza kutatua malalamiko ya wafanyakazi.
 ”Kama tunavyofahamu baraza la majadiliano ya pamoja katika utumishi wa umma ni chombo kilichoundwa kwa sheria ya bunge namba 19 ya 2003 ambayo ina lengo la kuimarisha mahusiano  na mawasiliano yenye tija baina ya serikali na halmashauri ambazo hazijaunda mabaraza hayo kuhakikisha zinayaunda, nay ale ambayo yamemaliza muda wake wanachaguliwa wajumbe wapya na kuhakikisha mabaraza yote yanakaa vikao ili kuweza kutatua malamiko ya wafanyakazi”alisema waziri.
Akasema kuwa baraza la majadiliano katika sekjta ya serikali za mitaa ni chombo halali  kwa mjibu wa kifungu namba 4 (10) ( c) cha sheria iliyoanzisha baraza hilo la majadiliano ya pamoja katika utumishi wa Umma.

 Waziri,Ghasia, amesisitiza  usimamizi wa rasilimali watu katika Sekta za Umma ni suala linalotakiwa kupewa kipaumbele kwani matumizi mazuri ya rasilimali watu ndiyo yanayoweza kuleta matokeo mazuri katika kusimamia rasilimali nyingine zote.
 Hivyo wanalo jukumu la msingi  la kuhakikisha wanatoa ushauri kwa serikali na watumishi a sekta hiyo ili kuongeza ufanisi  wenye  tija katika kuwahudumia wananchi hivyo watumie kikao hicho kuainisha maeneo yenye changamoto zaidi kwa watumishi ili kuondoa manung’uniko ya watumishi.
 Awali mwenyekiti wa baraza hlo jipya la kitaifa, Paulo Chikila, amesema kuwa Baraza hilo litakuwa madarakani kwa kipindi cha miaka mitatu akasisitiza kuwa mabaraza yote lazima yafanye kazi ili kuondoa malamiko ya wafanyakazi
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top