Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SABABU ZA TIMU YA TAIFA STARS KUSHINDWA ZATAJWA .... SABABU ZENYEWE HIZI HAPA

 


 
Taifa-StarsNA BELINDA KWEKA-MAELEZO
MAASKOFU na Wachungaji wa Good News For All Ministry watoa sababu ya Timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ kukosa ushindi katika mechi yao naTimu ya Ivory Coast iliyofanyika jumapili iliyopita Juni 16, mwaka huu.
 
Akizungumza na waandishi wa   habari leo(jana) katika ukumbi wa mikutano wa Idara ya Habari – MAELEZO  jijini da res salaam, Askofu Charles Gadi amesema kuwa kuna sababu nyingi zilizopelekea Taifa Stars kushindwa katika mchezo wake na Ivory Coast ikiwa ni pamoja na matusi na mzaha unaofanywa na wananchi wenyewe.
 
“Ndugu waandishi, ni kweli goli la kwanza lilifungwa kwa maombi ya Watanzania waliokuwa wakiomba, lakini matusi yaliyoendelea pale uwanjani ambayo yanatukana maumbile ya mama, dada, wakwe na watoto zetu wa kike yalitukwamisha.
 
“ Unapotukana kwa kutumia maumbile ya wakina mama ni sawa na kuchafua,kujeli uumbaji wa Mungu kwa wakina mama. Hali hiyo hutuletea laana ya kushindwa,” alisema Askofu Gadi.
 
Aliongeza kuwa walianza kuiombea Taifa Stars toka mwaka 2012 ili ifanikiwe katika mechi zake zote hivyo wana uchungu kwa kufungwa na timu hiyo ya kigeni.
 
Aidha Askofu Gadi aliongeza kuwa pale uwanjani kulikuwa kumefurika watu wengi hivyo kuhatarisha usalama wa watu walioko pale na hivyo ameiomba  Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litoe tiketi kulingana na idadi ya viti vilivyopo uwanjani.
 
Pia Askofu Gadi amesema kuwa wana maombi ya siku elfu moja kwa ajili ya kuliombea Taifa zima, mpaka sasa wamekaribia siku mia tano katika maombi  hayo hivyo wanaomba watu kutokwamisha maombi yao kwa kuacha matusi.
 
“Naomba Watanzania wamwogope Mungu kwa kuacha matusi na dhambi zao kwani wakifanya hivyo nchi itakuwa na maendeleo na kuwa ya kistaarabu kwa kuendeleza amani,” alisisitiza Mchungaji Leonard Kijuna.
 
Pia Askofu Gadi ametoa wito kwa Serikali kuwa waweze kutunga sheria kuhusu matusi kwamba endapo mtu atapatikana akitukana basi achukuliwe hatua kama zilivyo nchi njingine,mtu akitupa bigijii anafungwa, kwani  itasaidia kutokomeza kabisa suala hilo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top