Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

AGIZO LATOLEWA KWA WAVUNJIFU WA AMANI NCHINI

 


Picture 011
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi
Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayosimamia ofisi za Viongozi wakuu wa kitaifa imelipongeza Jeshi la Polisi kwa jinsi linavyotekeleza majukumu yake kwa kuwachukulia hatua wachochezi wanaotumia  mgongo wa siasa au dini hapa nchini.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mh. Hamza Hassan Juma aliyasema hayo jana wakati wa ziara ya kamati hiyo ilipotembelea makao makuu ya Jeshi la Polisi kwa lengo la kujifunza na kuweka mikakati ya pamoja katika kukabiliana na uhalifu pamoja na kuboresha maisha ya askari Polisi.
Alisema, Jeshi la Polisi linapaswa kutomuonea muhali mtu yeyote ama taasisi itakayotumia mwamvuli wa siasa au dini kupandikiza na kueneza chuki ndani ya jamii kitendo ambacho hupelekea uvunjifu wa amani.
Aidha, Mwenyekiti wa kamati hiyo, alishauri kuwa viwanja vyote vinavyomilikiwa na Jeshi la Polisi vipatiwe hati miliki ili kupunguza uvamizi katika maeneo na viwanja vya Polisi na endapo kuna wavamizi wowote wachuliwe hatua za haraka.
Kwa upande wake Kamishina wa operesheni na mafunzo wa Jeshi la Polisi (CP) Paul Chagonja  alibainisha matishio yanayoikabili nchi kwa sasa ambayo ni misimamo mikali ya kisiasa, migogoro ya wafugaji na wakulima, biashara ya dawa za kulenya, mauaji yanayosababishwa na imani za kishirikina na watu kuwania mali pamoja na ajali za barabarani zinazosababisha vifo kutokana na waendesha pikipiki na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi limejipanga na linaendelea na mikakati mbalimbali ya kiusalama katika kukabiliana na matishio hayo ikiwemo kupeleka askari  katika tarafa ili kuimarisha ulinzi ngazi ya tarafa hadi familia.
Aidha, aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kuwafichua wahalifu waliopo kwenye jamii kabla hawajatekeleza adhima yao ya kutenda uhalifu.
Aliongeza kuwa hivi sasa Jeshi hilo linaendelea kutekeleza program ya maboresho ili kuboresha  vitendea kazi pamoja na maslahi ya askari ambapo kila askari hivi sasa pamoja na mambo mengine anapata matibabu kwa kutumia bima ya afya na zaidi ya shilingi bilioni 42 zimekopeshwa kwa askari kupitia chama cha ushirika cha kuweka na kukopa cha Jeshi la Polisi ( Ura Saccos) kwa lengo la kuboresha maisha ya askari binafsi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top