Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mbunge wa Kitope atembelea Miradi ya Jimbo hilo


 

 Mbunge wa Jimbo la  Kitope Balozi Seif akikabidhi msaada wa Bati kwa ajili ya kusaidia uwezekaji wa Jengo la Klabu ya Soka ya Timu ya Kombora iliyopo Kitope.
Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Kirombero Mwalimu Juma Simai akipokea msaada wa vifaa vya kupikia chai vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi kwa skuli zote za jimbo hilo.Hafla hiyo imefanyika katika uwanja wa michezo wa Kombora Kitope.
 Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi akizindua na kukagua kisima cha maji safi kiliopo Kijiji cha Mgambo ambacho kimejengwa  kutokana na Mfuko wa Jimbo la  Kitope.
Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi msaada wa Magodoro, Juzuu na Mashaf Ustadhi wa Madrasat Qiyamu Islamia ya Mgambo Wilaya ya Kaskazini Unguja,akitekeleza ahadi aliyoipa Madrasa hiyo.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar na Mbunge wa Kitope Balozi Seif. Ali Iddi, akizungumza na Wanafunzi wa Madrasat Qiyamu Islamia ya Mgombo Unguja ili kufanya bidii katika  kusoma na ili kuja kuwa Walimu Bora wa baadae wa Elimu ya Dini ya Kiislam,(Picha na Hassan Issa  – OMPR)


Na Othman Ame OMPR.
Walimu wa Madrasa wameaswa kujiepusha na tabia ya  kuwafundisha  watoto ushabiki wa Kisiasa  kwa kutumia  mafundisho ya Dini  jambo ambalo linaweza kuleta matabaka  na ni hatari kwa watoto hao katika maisha yao ya baadaye.

Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi alitoa nasaha hizo wakati wa hafla fupi ya Kukabidhi msaada wa Magodoro, Misahafu, Juzuu pamoja na fedha taslimu kwa ajili ya ununuzi wa mpira wa kusambazia maji kwa Madrasat  Qiyamu Islamia hafla iliyofanyika katika uwanja wa Skuli ya Mgambo Wilaya ya Kaskazini “ B “.

Balozi Seif ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema jamii katika baadhi ya maeneo Nchini imekuwa ikikosa utulivu wa kimaisha na hatimae kuingia katika mgongano  baina ya jamii kutokana na baadhi ya walimu kuendeleza hulka ya kushawishi wanafunzi wao kujihusisha na masuala ya Kisiasa.

Alisema wakati umefika kwa walimu hao kuhakikisha kwamba wanasimamia vyema ufundishaji sahihi uliosisitizwa katika Qurani pamoja na  maamrisho yote yaliyomo ndani ya mfumo mzima wa Dini ya Kiislamu.

Aliwataka waalimu na wananchi kuendelea kuwa na subra hasa wakati wanapoomba nguvu za ziada za kupatiwa misaada katika miradi yao ya maendeleo na hata ile ya Kidini.
 
Credit: Zanzinews
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top