Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

LIGI KUU: SIMBA VS YANGA, AZAM VS JKT RUVU, PRISONS VS ASHANTI MECHI TAMU, RATIBA NZIMA HII HAPA!!

 



IMG_3703

PAZIA la ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014 linafungwa kesho aprili 19 kwa timu zote 14 kushuka uwanjani katika miji tofauti nchini.

Ligi inamalizika kesho wakati timu tatu zimeshajihakikishia nafasi tatu za juu.

Azam fc wametwaa ubingwa baada ya kufikisha pointi 59 ambazo haziwezi kufikiwa na klabu yoyote.

Yanga wamechukua nafasi ya pili wakiwa na pointi 55 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote chini yake.

Mbeya City nao wameshika nafasi ya tatu kwa pointi 46 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote ya chini yake.

Simba sc wao wao wapo mbioni kuisaka nafasi ya nne kwa pointi zao 37 baada ya kucheza mechi 25.




Nafasi ya tano wapo Kagera Sugar wenye pointi 35, na endapo Simba watafungwa kesho na wao wakashinda, basi Mnyama anaweza kumaliza ligi katika nafasi ya tano.

Katika mechi zote 7 hapo kesho, mechi tatu pekee  zina  hamasa kubwa kwa mashabiki wa soka nchini.

Mechi ya kwanza iliyovuta hisia za mashabiki wa soka ni ile ya Yanga dhidi ya Simba sc ndani ya uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Timu hizi zitakutana zikiwa na mafanikio tofauti msimu huu ambapo Yanga wameambulia nafasi ya pili, huku Mnyama akijikongoja katika nafasi ya nne.

Simba na Yanga zinakutana jumamosi, huku Yanga wakiwazidi wenzao kwa mafanikio msimu huu.
Na Baraka Mpenja wa fullshangwe, Dar Es Salaam
0712461976

Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top