Baadhi
ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakiwasili katika Ukumbi wa
Mikutano kwa ajili ya kuendelea kujadili Sura ya Kwanza na Sita ya
rasimu ya Katiba Mpya leo mjini Dodoma
Wauguzi
na Waganga wa Zahanati ya Bunge mjini Dodoma wakitoa msaada wa huduma
ya kwanza na kufanya maandalizi ya kumpeleka Mjumbe wa Bunge Maalum la
Katiba Ziana Mohamed Haji katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma leo baada
ya kupata matatizo ya mshutuko.
Wajumbe
wa Bunge Maalum la Katiba ambapo pia ni Ndugu na Jamaa wa Mjumbe wa
Bunge hilo Ziana Mohamed Haji wakijadiliana na watendaji wa Bunge hilo
jinsi ya kumsaidia baada ya kupata matatizo ya mshutuko leo mjini
Dodoma. Makamu
wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambaye pia ni Mjumbe
wa Bunge Maalum la Katiba Balozi Seif Ally Idd(katikati) akibadilishana
mawazo na Wajumbe wa Bunge hilo Mohamed Aboud Mohamed(kushoto) na Haji
Omar Heri (kulia) leo mjini Dodoma wakati mapumziko mafupi ya mjadala
kuhusu Sura ya Kwanza na Sita ya rasimu ya Katiba mpya.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge
Maalum la Katiba Mizengo Pinda (kulia) akibadilishana mawazo na Wajumbe
wenzake Mohamed Aboud Mohamed(katikati) na Dkt. Tereza Huvisa(kushoto)
leo mjini Dodoma wakati wa mapumziko mafupi ya kujadili Sura ya Kwanza
na Sita ya rasimu ya Katiba mpya.
Mjumbe
wa Bunge Maalum la Katiba Saada Mkuya Salum akichangia maoni yake leo
mjini Dodoma kuhusu Sura ya Kwanza na Sita ya rasimu ya Katiba mpya.
Picha na Ofisi ya Bunge Maalum la Katiba
Post a Comment