Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

BAN KI MOON ACHUKIZWA NA VITA NCHINI SYRIA


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon (pichani) ametoa wito kwa nchi wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kuacha tofauti zao na kumuunga mkono mjumbe wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu Lakhdar Brahimi, katika juhudi zake za kuusuluhisha mgogoro wa Syria.
Katika hotuba yake mbele ya baraza kuu la Umoja wa Mataifa, Bw. Ban Ki-Moon amezitahadharisha nchi wanachama kwamba hali nchini Syria imezorota kupita kiasi.
Amesema ukatili mkubwa na ukiukaji wa haki za binadamu unaendelea, ukifanywa hasa na upande wa serikali, lakini na upande wa waasi pia.
Shirika la kuchunguza haki za binadamu nchini Syria lenye makao nchini Uingereza, linakadiria kwamba watu wapatao 30,000 wamekwishauawa nchini humo tangu mgogoro huo ulipoanza takriban miezi 18 iliyopita.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top