Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MISS TANZANIA 2012 KUFANYIKA BLUE PEARL HOTEL, UBUNGO NOVEMBA 3

Mkurugenzi wa Lino International Agency (kushoto) akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) asubuhi hii, kutaja tarehe ya kufanyika shindano la Miss Tanzania 2012, ambayo ni Novemba 3, mwaka huu katika ukumbi wa Blue Pearl Hotel, Ubungo Plazza, Dar es Salaam. Kushoto ni Miss Tanzania 2011, Salha Israel. Lunedenga amesema washiriki wote wa Miss Tanzania wataingia kambini Oktoba 2 katika hoteli ya Girraffe, iliyopo Mbezi, Dar es Salaam ambako watakaa kwa mwezi mmoja kuelekea shindano hilo, wakinolewa na walimu waliobobea, akiwemo Salha.
Mratibu huyo alisema kuwa mashindano ya mwaka huu yanaonekana kuwa na ushindani zaidi kutokana na kanda mbalimbali kutoa warembo wenye vigezo vinavyokaribiana jambo lililowapa majaji wakati mgumu wa kufanya maamuzi.
Mapema mwaka huu, Kamati hiyo iliendesha shindano dogo na kumpata Lissa Jensen ambaye aliwakilisha nchi katika fainali za Dunia kutokana na mabadiliko ya kalenda yaliyofanywa na Kamati ya Miss World na mrembo atakayetwaa taji hilo katika fainali hizo zitakazofanyika hivi karibuni atapata muda mrefu wa kufanya maandalizi.
Shindano la Miss Tanzania lilianza rasmi mwaka 1994 na Aina Maeda alikuwa mshindi wa kwanza, akifuatiwa na Shose Senare 1995, Emily Adolf 1996, Saida Kessy 1997, Basila Mwanukuzi 1998, Hoyce Temu 1999, Jacqueline Ntuyabaliwe 2000, Happiness Magese 2001, Angela Damas 2002, Sylvia Bahame 2003, Faraja Kotta 2004, Nancy Sumary 2005, Wema Sepetu 2006, Richa Adhia 2007, Nasreem Kareem 2008, Miriam Gerald 2009, Geneveive Mpangala 2010 na Salha Israel 2011.
Awali ya hapo, mwaka 1967 lilifanyika shindano la kwanza kabisa la Miss Tanzania na Theresa Shayo akashinda katika shindano lililofanyika kwenye bwawa la kuogelea la hoteli ya Kilimanjaro, lakini serikali ya Tanzania wakati huo, chini ya rais wa kwanza, hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikapiga marufuku mashindano kwa sababu hayaendani na mila na desturi za Mtanzania.
Lakini Lino International Agency, ikajenga hoja ambazo ziliishawishi serikali ya Tanzania, chini ya rais wake wa pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi kuruhusu mashindano hayo yafanyike tena, ingawa mwaka 2001 yaliponea chupuchupu kufutwa tena, enzi za rais wa awamu wa tatu, Benjamin William Mkapa.
Ilitokana na vazi la kuogelea ‘kichupi’, ambalo lilipingwa kwa sababu linamdhalilisha mwanamke wa Tanzania, lakini Lino ikaboresha kipengele cha vazi hilo, kutoka la kuogelea hadi la ufukweni, ambalo kidogo linamsitiri binti na serikali ikaruhusu mashindano yaendelee.
Hata hivyo, mabinti wanapokwenda kwenye shindano la dunia, wanavaa vazi la kuogelea kupanda jukwaani, katika shindano ambalo linaonyeshwa moja kwa moja nchi zaidi ya 100 duniani na picha zao kuchapishwa kwenye majarida, magazeti na mitandao mbalimbali duniani. 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top